Picha hii haihusiki na ajali ya basi la Zuberi iliyotokea mchana huu huko wilayani Ikungi.
Mwandishi wetu, Ikungi
BASI
 la Zuberi lenye namba T119 AA2 limepata ajali mbaya katika kijiji cha 
Nkuhi wilaya ya Ikungi Mkoa wa Singida na watu wanne wameripotiwa kufa 
papo hapo kwa kukatwa vichwa huku majeruhi wengi wakiwa wameumia vibaya 
sehemu mbalimbali za mwili.
Akizungumza
 na MOblog kutoka eneo la tukio leo mchana huu, mwandishi wa habari, 
Nathanieli Limu  amesema basi hilo la Zuberi lilikuwa linatoka Mwanza 
kuja Dar na lilikuwa na zaidi ya abiria 60.
Amesema
 kuwa chanzo cha ajali ni dereva wa basi hilo alikuwa anajaribu kumkwepa
 bibi kizee aliyekuwa anakatisha barabarani kwenye majira ya saa saba 
mchana.
“ilikuwa
 si ajali ya kawaida baada ya bibi kizee kukatiza barabarani na wakati 
dereva anajaribu kumkwepa alirudi mara ya pili barabarani ndipo hapo 
gari lilipinduka na kuanguka kwenye mtaro,” amesema Limu
Alilisitiza
 kwamba mashuhuda wa ajali hiyo wanahusisha tukio hilo na imani za 
kishirikiana baada ya bibi huyo kuamua kurudi mara ya pili barabarani na
 kusababisha ajali na kukaa kwa muda mrefu eneo la tukio.
Amesema
 kwa basi hilo la Zuberi liliinuliwa na lori lenye kifaa maalumu cha 
winch baada ya basi hilo kumlalia mtoto mdogo wa miezi kadhaa ambaye 
mama yake ni miongoni mwa waliofariki dunia papo hapo na maiti yake 
kupelekwa hospitali ya mkoa wa Singida.
Chanzo: Mo blog 
0 comments:
Post a Comment