Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Polisi Mkoa wa Singida, wanamshikilia Jafari Hamisi (23),Mkazi 
wa Ukombozi mjini Singida,kwa tuhuma ya kumilki kinyume cha sheria 
vipande 16 vya meno ya ndovu vyenye thamani ya zaidi ya Sh17milioni.
Meno hayo yamekamatwa ikiwa ni siku nne toka meno 
mengine vipande 21 vyenye thamani ya zaidi ya Sh43 milioni,kukamatwa 
kwenye eneo lile lile la kizuizi cha mazao kilichopo katika Kijiji cha 
Ukimbu kata ya Mgandu Wilaya ya Manyoni.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake 
jana,Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida.SSP.Cordula Lyimo,alisema 
meno hayo yamekamatwa Feb 16 mwaka huu saa tano usiku katika kizuizi cha
 mazao kilichopo Kijiji cha Ukimbu,Kata ya Mgandu Tarafa ya Itigi Wilaya
 ya Manyoni.
Alisema askari wakiwa katika kizuizi 
hicho,walifanya ukaguzi kwenye gari T.288 AJF aina ya Scania mali ya 
Kampuni ya Super Service likiendeshwa na Ally Hamadi,likitokea 
Makongorosi Chunya,kuelekea Itigi Wilaya ya Manyoni.
“Baada ya upekuzi huo,walikuta meno hayo yakiwa 
yamehifadhiwa ndani ya begi la nguo na kuwekwa kwenye keria za ndani ya 
basi.Mtuhumiwa aliweza kupatikana wakati akiwa katika juhudi za kutaka 
kutoka ndani ya basi ili akimbie”,alisema Lyimo.
Kaimu kamanda huyo,alisema uchuguzi zaidi 
unaendelea ili kubaini au kupata mtandao kamili unaojihusisha na kuwinda
 pamoja na kununua nyara hizo.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment