Home » » Ashikiliwa kwa nyara za Serikali

Ashikiliwa kwa nyara za Serikali

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Polisi Mkoa wa Singida, wanamshikilia Jafari Hamisi (23),Mkazi wa Ukombozi mjini Singida,kwa tuhuma ya kumilki kinyume cha sheria vipande 16 vya meno ya ndovu vyenye thamani ya zaidi ya Sh17milioni.

Meno hayo yamekamatwa ikiwa ni siku nne toka meno mengine vipande 21 vyenye thamani ya zaidi ya Sh43 milioni,kukamatwa kwenye eneo lile lile la kizuizi cha mazao kilichopo katika Kijiji cha Ukimbu kata ya Mgandu Wilaya ya Manyoni.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana,Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida.SSP.Cordula Lyimo,alisema meno hayo yamekamatwa Feb 16 mwaka huu saa tano usiku katika kizuizi cha mazao kilichopo Kijiji cha Ukimbu,Kata ya Mgandu Tarafa ya Itigi Wilaya ya Manyoni.
Alisema askari wakiwa katika kizuizi hicho,walifanya ukaguzi kwenye gari T.288 AJF aina ya Scania mali ya Kampuni ya Super Service likiendeshwa na Ally Hamadi,likitokea Makongorosi Chunya,kuelekea Itigi Wilaya ya Manyoni.
“Baada ya upekuzi huo,walikuta meno hayo yakiwa yamehifadhiwa ndani ya begi la nguo na kuwekwa kwenye keria za ndani ya basi.Mtuhumiwa aliweza kupatikana wakati akiwa katika juhudi za kutaka kutoka ndani ya basi ili akimbie”,alisema Lyimo.
Kaimu kamanda huyo,alisema uchuguzi zaidi unaendelea ili kubaini au kupata mtandao kamili unaojihusisha na kuwinda pamoja na kununua nyara hizo.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa