Home » » Diwani kortini kwa lugha chafu

Diwani kortini kwa lugha chafu

 DIWANI wa Unyambwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Singida, Shabani Salumu (CCM), amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya mjini Singida, akikabiliwa na tuhuma za kuwatolea lugha ya matusi maofisa wa polisi ikiwemo kudai ni ‘mizigo’.
Mbele ya Hakimu Aisha Mwetindwa, Mwendesha Mashitaka, Chemu Mussa, alidai  kuwa Januari 12, mwaka huu, saa 1.30 asubuhi katika Kijiji cha Ijanuka, Kata ya Unyambwa,  mshitakiwa aliwatolea lugha ya matusi maofisa wa polisi kitendo kilichoelekea kusababisha kutoweka au kuvunjika kwa amani.
Alidai tukio hilo lilitokea wakati maofisa hao wakiwa kazini kwenye eneo ambalo wananchi wa Kata ya Unyambwa walichoma moto basi la Kampuni ya Mtei.
Mshitakiwa alikana tuhuma hizo na yupo nje kwa dhamana. Kesi itatajwa Februari 25, mwaka huu.
Chanzo;Tanzania 
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa