Home » » TANGASIS WASUSIA FIDIA KIDUCHU

TANGASIS WASUSIA FIDIA KIDUCHU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WAKAZI wa Mwambani, Kata ya Tangasisi, wilayani Tanga wameelezea kutoridhishwa na fidia waliyolipwa ili kupisha ujenzi wa reli kwenye Bandari mpya ya Mwambani.
Wakazi hao zaidi ya 200 wanaoishi kandokando ya bahari wamelipwa sh 3,400 kwa mita moja ya mraba wakati viwango vya jiji hilo kwa sasa ni sh 7,000 kwa ukubwa huo kitu kinachowafanya wadai fidia zaidi.
Kwa sababu hiyo wamemuomba Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe na Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, kuingilia kati suala hilo kwa kuwa thamani ya pesa wanayolipwa hailingani na mali zao.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa