Home » » Akamatwa na vipande 21 vya meno ya tembo

Akamatwa na vipande 21 vya meno ya tembo

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


JESHI la Polisi limemkamata mtu mmoja  mkazi wa Mwamagembe, Itigi wilayani Manyoni, Singida, George James (30)  na vipande 21 vya meno  ya tembo akiwa njiani kuvisafirisha.
Kamanda wa Polisi mkoani humo (SACP) Geofrey Kamwela, alisema jeshi hilo lilifanikiwa kumkamata kijana huyo baada ya kuweka mtego wakati wakiwa ndani ya gari.
Alilitaja gari hilo kuwa ni Toyota Hiace lenye namba za usajili T 797 CQL wakati akiwa katika harakati za kusafirisha meno hayo  kwenda Itigi mjini.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa