Mkuu
 wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone,(wa kwanza kushoto) akipata maelezo
 kutoka mkandarasi wa daraja la Mwankoko manispaa ya Singida,Rogers 
Mchau(anayenyoosha mkono) juu ya maendeleo ya ujenzi wa daraja kijiji 
cha Mwankoko.
Dk.Kone
 alilikagua daraja hilo baada ya kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa, 
kulalamika kwamba fedha zinazotumika katika ujenzi huo ni nyingi 
hazifanani na daraja lenyewe. Baada ya kulikagua,alikiri kuwa daraja 
hilo lina thamani na fedha zilizotumika na kwamba bado kuna zaidi ya 
shilingi 192 milioni zinahitajika ili kukamilisha ujenzi huo.
Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone,akikagua ujenzi wa daraja la kijiji cha Mwankoko manispaa ya Singida.
Mkuu
 wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone, akitoa maelekezo juu ya kuboresha 
ujenzi wa daraja la kijiji cha Mwankoko manispaa ya Singida.
Daraja la kijiji cha Mwankoko linaloendelea kujengwa na mkandarasi Rogers Mchau.
Mkuu
 wa mkoa wa Singida (kushoto) akizungumza na Meya Mstahiki wa manispaa 
ya Singida,Sheikh Salum Mahami wakati alipokuwa akimaliza kukagua ujenzi
 wa daraja la kijiji cha Mwankoko.(Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
MKUU
 wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone,ameipongeza Halmashauri ya Manispaa 
ya Singida,kwa juhudi zake za kujenga daraja linalolingana na thamani ya
 fedha iliyotumika.
 Dk.Kone
 ametoa pongezi hizo mwishoni mwa wiki wakati akikagua ujenzi wa daraja 
hilo, ulioanza rasmi desemba 12 mwaka 2011 na ulitarajiwa kukamilika 
novemba 14 mwaka 2012.Daraja hilo linaunganisha kata ya Mwankoko na kata
 ya Mtamaa.
Amesema
 kuwa fedha ambayo imetumika hadi sasa ya zaidi ya shilingi 216.1 
milioni,thamani ya fedha hiyo inafafanana kabisa na kazi ya ujenzi 
iliyofanyika.
 “Kwa
 kweli mmefanya kazi nzuri pamoja na mkandarasi wenu.Fedha ambazo 
mmeziomba serikali kuu ili mmalizie ujenzi wa daraja hili,tutakuwa nyuma
 yenu katika kuhakikisha mmezipata,ili ujenzi uweze kukamilika kwa 
mujibu wa mkataba wenu”,amesema.
Mapema
 Mkurugenzi wa Manispaa hiyo,Joseph Mchina,amesema mradi huo wa ujenzi 
wa daraja hilo,fedha zake zimetoka katika mfuko wa barabara kupitia 
OWM-TAMISEMI,zikiwa ni fedha za maombi maalum ya ujenzi wa madaraja.
 Katika
 hatua nyingine,Mchina amesema hadi sasa ujenzi huo wa 
daraja,umekamilika na magari yameanza kulitumia kwa tahadharai,kwani 
bado kuna kazi ambazo hazijakamilika.
 Mkurugenzi
 huyo alitaja baadhi ya kazi ambazo bado hazijakamilika kuwa ni ujenzi 
wa barabara ya kuingia na kutoka,mifereji ya wazi kandokando ya barabra 
ya kuingia na kutoka na kuweka alama barabarani.
 Alitaja
 kazi zingine ambazo bado hazijakamilika,kuwa ni pamoja na kazi ya 
ujenzi wa kuta za kulinda daraja,kuweka bomba za pembeni na kuweka nguzo
 za kuonesha mwlekeo wa daraja.
 “Katika
 mwaka wa fedha wa 2014/2015,halmashauri ya manispaa,imeomba kiasi cha 
shilingi 200 milioni kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huu”,amesema.
Mkuu
 huyo wa mkoa,amelazimika kukagua mradi huo wa ujenzi wa daraja,baada ya
 ujenzi huo kulalamikiwa kuwa umetumia fedha nyingi ambazo hazilingani 
na kazi iliyofanyika.Mbaya zaidi ni kwamba ujenzi huo upo nyuma ya muda 
kwa mujibu wa mkataba.
Mo Blog 
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment