Home » » RC Singida ahimiza ushirikiano

RC Singida ahimiza ushirikiano

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Parseko Kone, amewataka wakazi wa Kanda ya Kati kutoa taarifa sahihi kwa wadadisi na wahariri wa utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi, ili Serikali iweze kutambua hali halisi ya ajira nchini. Dk Kone alitoa wito huo juzi wakati akifungua mafunzo ya wadadisi na wahariri wa utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi wa mwaka 2014. Alisema utafiti huo ambao mahojiano yake yanatarajiwa kufanywa katika kaya 11,520 nchini, unatarajiwa kuanza Februari mwaka huu na kwamba utatoa viashiria muhimu ikiwemo kujua hali ya ajira nchini.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa