Home » » MBEGU NA PEMBEJEO BORA VYACHANGIA ONGEZEKO LA UZALISHAJI WA ALZETI SINGIDA

MBEGU NA PEMBEJEO BORA VYACHANGIA ONGEZEKO LA UZALISHAJI WA ALZETI SINGIDA

MATUMIZI mbegu bora na pembejeo nyingine za kilimo pamoja na kuzingatia ushauri wa wataalamu, vimetajwa kusaidia kuongeza mara dufu kiwango cha uzalishaji wa zao la alzeti mkoani Singida.
Mtaalamu wa kilimo cha zao hilo  kutoka  halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida bwana Elias Ziwa amebainisha hayo katika  taarifa yake juu  ya mafanikio na changamoto za  kilimo cha Alizeti
Amesema  kuwa uzalishaji alzeti ambayo  ndio zao kuu la biashara kwa wakazi wa mkoa huo,  umeongezeka kutoka  magunia 4 kwa ekari miaka mitano iliyopita, hadi kufikia zaidi ya gunia  12 hivi sasa.
Hata  hivyo amesema pamoja na ongezeko hilo amesema wameweka mkakati  wa kuendelea kutoa elimu zaidi ili kufikia hatua  ya  baadhi ya wakulima waliofanikiwa kuvuka kiwango hicho cha uzalishaji alzeri kwa ekari gunia 15.
Kilimo cha alzeti  ndio  zao kuu la biashara kwa wakazi wa mkoa wa Singida  wapatao  milioni moja na laki tano,  ambapo takwimu zinaonesha kuwa zaidi ya tani 180,000 za zao hilo huzalishwa kwa mwaka.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa