MATUMIZI mbegu bora na
pembejeo nyingine za kilimo pamoja na kuzingatia ushauri wa wataalamu,
vimetajwa kusaidia kuongeza mara dufu kiwango cha uzalishaji wa zao la alzeti
mkoani Singida.
Mtaalamu wa kilimo cha zao hilo 
kutoka  halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida bwana Elias Ziwa
amebainisha hayo katika  taarifa yake juu  ya mafanikio na changamoto
za  kilimo cha Alizeti
Amesema  kuwa uzalishaji alzeti
ambayo  ndio zao kuu la biashara kwa wakazi wa mkoa huo,  umeongezeka
kutoka  magunia 4 kwa ekari miaka mitano iliyopita, hadi kufikia zaidi ya
gunia  12 hivi sasa.
Hata  hivyo amesema pamoja na ongezeko hilo
amesema wameweka mkakati  wa kuendelea kutoa elimu zaidi ili kufikia
hatua  ya  baadhi ya wakulima waliofanikiwa kuvuka kiwango hicho cha
uzalishaji alzeri kwa ekari gunia 15.
Kilimo cha alzeti  ndio  zao kuu la
biashara kwa wakazi wa mkoa wa Singida  wapatao  milioni moja na laki
tano,  ambapo takwimu zinaonesha kuwa zaidi ya tani 180,000 za zao hilo
huzalishwa kwa mwaka.
0 comments:
Post a Comment