Mkuu
 wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi, akizungumza kwenye ufunguzi wa 
mafunzo ya wiki mbili ya wadadisi na wahariri wa utafiti wa watu wenye 
uwezo wa kufanya kazi katika mikoa ya Singida ,Dodoma, Tabora na 
Kigoma.Mafunzo hayo yanafanyikia kwenye ukumbi wa mikutano wa VETA mjini
 Singida.
Baadhi
 ya wadadisi na wahariri wa utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi 
katika mikoa ya Kigoma, Tabora, Singida na Dodoma wakiwa kwenye mafunzo 
ya wiki mbili yanayohusu utafiti huo unaotarajiwa kufanyika mapema mwezi
 ujao.
Mkuu
 wa wilaya ya Singida, Queen Mlozi (wa pili kulia) akiwa kwenye picha ya
 pamoja na wadadisi na wahariri wa utafiti wa watu wenye uwezo wa 
kufanya kazi katika mikoa ya Singida,Kigoma,Tabora na Dodoma na 
wakufunzi wao.(Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
MKUU 
 wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone amewataka wakazi wa kanda ya kati 
kutoa taarifa sahihi kwa wadadisi na wahariri wa utafiti wa watu wenye 
uwezo wa kufanya kazi ili serikali iweze kutambua hali halisi ya ajira 
nchini.
Dr.
 Kone ametoa wito huo hivi karibuni wakati akifungua mafunzo ya wadadisi
 na wahariri wa utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi wa mwaka 
2014.
Amesema
 utafiti huo ambao mahojiano yake yanatarajiwa kufanywa katika kaya 
11,520 nchini, unatarajiwa kuanza mapema mwezi ujao wa februari.
Dk.
 Kone amesema utafiti huo wa nguvu kazi nchini, utatoa viashiria muhimu 
ikiwemo kujua hali ya ajira nchini katika sekta rasmi na isiyo rasmi.
“Pia
 utatusaidia kujua kiwango cha ukosefu wa ajira, kiwango cha ajira isiyo
 timilifu, ajira mbaya, ajira hatarishi kwa watoto, hali ya kipato 
kutokana na ajira, matumizi ya muda na ajira mpya zilizozalishwa katika 
kipindi cha kuanzia mwaka 2006/ hadi 2013”,amesema.
Aidha
 Mkuu huyo wa mkoa katika hotuba yake ilisomwa kwa niaba yake na DC wa 
Singida, Queen Mlozi, amewahakikishia wananchi kwamba taarifa 
watakazotoa zitakuwa ni za siri na zitatumika tu kwa matumizi ya 
kitakwimu pekee.
Kutokana
 na umuhimu wa utafiti huo, Dk. Kone amewahimiza wananchi wa mikoa ya 
Singida, Dodoma, Tabora na Kigoma kutoa ushirkiano kama walivyoutoa 
wakati wa zoezi la sense la watu na makazi agositi 2012.
Kwa
 mujibu wa Dk. KOne jumla ya ajira 610,285 zimepatikana nchini 
kutokanana uwekezaji wa miradi mbali mbali ya maendeleo pamoja na 
uwekezajikatika sekta binafsi kati ya mwaka 2010 hadi mwaka jana.
0 comments:
Post a Comment