Mwito
 huo ulitolewa juzi na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Parseko Kone wakati 
akifungua semina ya siku mbili juu ya Soko la kukuza ujasiriamali 
iliyofanyika ukumbi wa Aqua Vitae mjini hapa.
Dk
 Kone alisema kuwa Soko la Hisa la Dar es Salaam kupitia kitengo chake 
kipya kijulikanacho kama “Soko la Kukuza Ujasiriamali”, ni suluhisho la 
upatikanaji wa mitaji kwa wajasiriamali kote nchini.
Alisema
 kuwa soko hilo litatoa suluhisho kwa changamoto zinazowakabili 
wajasiriamali katika upatikanaji wa uhakika wa mitaji ya muda mrefu kwa 
ajili ya kuendeleza biashara zao, jambo ambalo limekuwa likiwasumbua 
wajasiriamali na wafanyabiashara.
“Kwa
 hiyo basi, soko la kukuza ujasiriamali litasaidia kuleta msukumo wa 
utekelezaji sera mbalimbali za serikali zinazolenga kuondoa changamoto 
hizo na kuleta urahisi wa upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya kukuza 
biashara zao,” Dk Kone alisema.
Aidha,
 alieleza kuwa soko hilo linatarajiwa kulichangamsha soko kwa ujumla 
kupitia ongezeko la utoaji na uorodheshaji wa hisa, kupanua wigo na 
fursa za kuwekeza mitaji na kuongeza ari ya wananchi kujiwekea akiba.
Kwa
 mujibu wa mkuu wa mkoa huo, baadhi ya faida ziletwazo na soko hilo ni 
kupunguziwa kodi katika gawio, kusamehewa kodi kwenye ongezeko la 
thamani ya mtaji na ushuru wa stempu na punguzo kodi ya makampuni.
Chanzo;Habari Leo 
0 comments:
Post a Comment