Meneja
 wa shrika la SEMA, Ivo Manyanku,(wa kwanza kulia) akitoa taarifa yake 
ya ujenzi wa vyoo bora katika shule tano za msingi manispaa ya Singida 
kwa Naibu Waziri TAMISEMI (Elimu), Mh. Kassim Majaliwa (mwenye 
miwani).Vyoo hivyo vimegharimu zaidi ya shilingi 155 milioni.
Naibu Waziri TAMISEMI (Elimu) Mh. Kassim Majaliwa (aliyeipa kisongo kamera) akizindua rasmi ujenzi wa vyoo bora katika shule ya msingi Unyankindi.Vyoo hivyo bora vimejengwa kwa gharama ya shilingi 155 milioni na shirika la SEMA.Kushoto ni meneja wa SEMA. Ivo Manyanku.
Naibu Waziri wa TAMISEMI (Elimu),Kassim Majaliwa akikata utepe kuashiria ufunguzi wa matumizi ya vyoo bora vya shule ya msingi Unyankindi mjini Singida.Vyoo hivyo vimejengwa na shirika la SEMA kwa gharama ya shilingi 155 milioni.
Naibu Waziri TAMISEMI (Elimu) Mh. Kassim Majaliwa (aliyeipa kisongo kamera) akizindua rasmi ujenzi wa vyoo bora katika shule ya msingi Unyankindi.Vyoo hivyo bora vimejengwa kwa gharama ya shilingi 155 milioni na shirika la SEMA.Kushoto ni meneja wa SEMA. Ivo Manyanku.
Naibu Waziri wa TAMISEMI (Elimu),Kassim Majaliwa akikata utepe kuashiria ufunguzi wa matumizi ya vyoo bora vya shule ya msingi Unyankindi mjini Singida.Vyoo hivyo vimejengwa na shirika la SEMA kwa gharama ya shilingi 155 milioni.
Moja ya vyoo bora vya shule ya msingi Unyankindi manispaa ya Singida vilivyojengwa na shirika la SEMA la mkoa wa Singida.
Shirika
 lisilo la kiserikali la Sustainable Environment Management Action 
(SEMA) la mkoani Singida limetumia zaidi ya shilingi 155 milioni 
kugharamia ujenzi wa vyoo bora katika shule tano za manispaa ya Singida.
 Shule zilizonufaika na mradi huo ni,Unyankindi,Singidani,Manguamitogho,Mtamaa na Mtisi.
 Hayo 
yamesemwa juzi na Meneja wa SEMA, Ivo Manyanku wakati akizungumza kwenye
 hafla iliyofana ya uzinduzi wa vyoo hivyo uliofanyika katika shule ya 
msingi Unyankindi Singida mjini.
 Amesema
 fedha hizo zilizotumika katika ujenzi huo zimetolewa ufadhili na 
shirika la WaterAid Tanzania kwa ajili ya kutekeleza mradi wa maji na 
usafi shuleni katika halmashauri ya manispaa ya Singida.
 “Vyoo
 hivi vina matundu 48 ambayo yana uwezo wa kuhudumia wanafunzi 2,903 
kati yao wavulana ni 1,446 na wasichana ni 1,457.Idadi hiyo inajumuisha 
na walemavu 38 ambao 25 ni wavulana na 13 ni wasichana”,amesema Meneja 
huyo.
 Kwa 
upande wake mgeni rasmi katika uzinduzi huo,naibu waziri TAMISEMI 
(elimu),Kassimu Majaliwa,alitumia fursa hiyo kulipongeza shirika la SEMA
 kwa ujezi bora wa vyoo hivyo ambavyo vimekidhi vigezo vyote 
vinavyohitajika.
 Amesema
 serikali na wadau wengine wa maendeleo hawana budi kuliunga mkono 
shirika la SEMA kwa madai linatelekeza miradi yake kulingana na thamani 
ya fedha zilizotumika.
 “SEMA binafsi nawapongezeni sana ujenzi huu mtakuwa mmeisaidia serikali katika kupunguza 
kero
 mbalimbali zinazoikabili sekta mbalimbali ikiwemo ya elimu.Vyoo hivi ni
 bora mno na vitakuwa vimepunguza kwa kiwango kikubwa uhaba wa vyoo 
katika shule zetu za msingi”,amesema Majaliwa.
 Wakati
 huo huo, Naibu Waziri huyo ameuomba uongozi wa halmashauri ya manispaa 
ya Singida kusimamia matumizi ya vyoo hivyo ili viweze kutumika kwa muda
 mrefu zaidi.
Chanzo: Singida yetu  




0 comments:
Post a Comment