Home »
 » Matatani kwa kumbaka kikongwe 
 
Matatani kwa kumbaka kikongwe 
| 
 | 
 
  | 
 
 
 
  
    |  
      
       
      POLISI mkoani Singida      inamshikilia mkazi wa Kijiji cha 
Wibia, Saidi Hamisi (30) kwa tuhuma za      kumbaka bibi kizee mwenye 
umri wa miaka themanini, mkazi wa Kijiji cha      Matongo, Wilaya ya 
Ikungi, mkoani hapa. 
            Akizungumza na waandishi wa      habari ofisini kwake, 
kamanda wa jeshi hilo mkoani Singida, Kamishna      Msaidizi wa Polisi, 
Geofrey Kamwela, alisema tukio hilo lilitokea juzi      usiku na kumtaja
 aliyembaka bibi kizee huyo kuwa ni Saidi Hamisi. 
            Aidha, Kamanda Kamwela      alifafanua pia kwamba tukio hilo
 la ubakwaji wa bibi kizee huyo lilitokana      na ulevi wa kupindukia 
kwa mtuhumiwa. 
            Kamishna msaidizi huyo alisema      “mtuhumiwa alifanya 
kitendo hicho kutokana na kuwa wakiishi nyumba moja na      bibi huyo 
hivyo alipokunywa pombe na kulewa ndipo alipoona aende akamalize      
matatizo yake kwa jirani yake huyo,” alisema. 
            Kwa mujibu wa maelezo ya jamaa      wa karibu wa mtuhumiwa 
huyo, inasemekana kwamba baada ya mtuhumiwa kumaliza      kitendo hicho 
aliamua kuendelea kulala na bibi kizee huyo mpaka asubuhi ili      aweze
 kuendelea tena na kitendo hicho asubuhi kabla ya kuondoka kwenda      
kuendelea na shughuli zake nyingine. 
            Aidha, Kamanda Kamwela      alisisitiza kuwa majira ya saa 
7:15 usiku wananchi walitoa taarifa kwenye      kituo cha polisi ndipo 
jeshi hilo lilifanikiwa kumkamata mtuhumiwa na      kumhoji. 
            Kwa mujibu wa Kamanda Kamwela,      bibi kizee huyo 
amepelekwa hospitalini kwa uchunguzi zaidi ili kujiridhisha      iwapo 
amefanyiwa kitendo hicho cha kinyama na mjukuu wake na kama      
hajaambukizwa magonjwa ya zinaa. 
 
Chanzo;Tanzania Daima  
       
 |  
 
 | 
 
 
0 comments:
Post a Comment