Baadhi
 ya wananchi wakiwa wamehamishia makazi yao chini ya mti uliopo kwenye 
korongo kijiji cha Handa mpakani mwa Wilaya ya Chemba na Singida 
Vijijini mara baada ya nyumba zao kuchomwa moto na askari polisi na wale
 wa kikosi cha kupambana na ujangili kwa madai ya kuvamia hifadhi ya 
msitu wa mgori (PICHA NA HILLARY SHOO).
 Huyu
 ni mmoja wa watoto walionashwa na kamera yetu akiwa amelala hoi kwa 
kukosa chakula na huduma zingine, baada ya nyumba zao kuchomwa moto 
wakati wa operesheni ya kuwahamisha katika kitongoji cha Kazamoyo kwa 
madai ya kuvamia hifadhi, hata hivyo wananchi hao wameisha katika eneo 
hilo kwa zaidi ya miaka nane toka mwaka 2005 , lakini sheria ya kuingiza
 eneo hilo kwenye msitu wa hifadhi ya mgori ilifanyika mwaka 2007, 
(PICHA NA HILLARY SHOO).
.Unyanyasaji dhidi ya wananchi wakithiri wilayani Singida 
Na Hillary Shoo, Singida
KITUO
 cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) wametakiwa kufika katika 
kitongoji cha Kazamoyo kijiji cha Nguamuhanga tarafa ya Mgori Wilayani 
Singida vijijini na kujionea unyanyasaji dhidi ya wananchi wakati wa 
zoezi la kuwaondoa katika hifadhi ya msitu wa mgori.
Hayo
 yamesemwa juzi katika kitongoji hicho na baadhi ya wananchi walioamua 
kuhamia kwenye korongo na kuishi chini ya miti kama digidigi kunusuru 
maisha yao kutokana na vipigo kutoka kwa wa kikosi cha kupambana na 
ujangili Wilaya ya Singida na askari polisi.
Wamesema
 ni vyema kituo hicho wakafika mapema ili kuona jinsi ambavyo binadamu 
wanavyoishi maisha ya shida ta taabu kwenye eneo hilo kufuatia amri ya 
mkuu wa Wilaya ya kuhamisha kwa muda mfupi.
Wamesema
 eneo hilo wameishi zaidi ya miaka nane na kujenga makazi bora bila 
matatizo yoyote, lakini jambo la ajabu ni baada ya Wilaya ya Chemba na 
Sngida kuwekeana mipaka na kuonekana kuwa wako Singida.
“Wakati
 tuko kijiji cha Handa Wilaya ya Chemba, tuliishi bila matatizo lakini 
baada ya kuhamia singida ndipo mambo yalianza kubadilika na kuambiwa 
kuwa tuko eneo la hifadhi, hii ni ajabu sana , Wilaya moja tuliishi 
vizuri hii nyingine haitutaki sasa tuende wapi.” Alihoji mmoja wa kina 
mama.
Licha
 ya kukosa huduma muhimu kama vile maji, mahema, vyoo baadhi ya kina 
mama na watoto walionekana wakiwa katika huzuni klubwa huku wengine 
wakiangua vilio baada ya kuwaona waandishi wa habari wakidhani kuwa ni 
askari.
Hata
 hivyo eneo hilo lina mbu wengi, jua kali na mbaya zaidi hivi sasa ni 
msimu wa mvua katika maeneo hayo, je swali la kujiuliza wataishije hapo 
wananchi hao zaidi ya 1,000 ambao nyumba zao zimechomwa moto.
Hata
 hivyo Mkuu wa Wilaya ya Singida Qeen Mlozi amesema zoezi hilo 
linaendelea sanjari na kuhakikisha wanaondoka kwenye korongo hilo 
walimojificha.
Hivi
 karibuni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu 
alitembelea eneo hilo la kusitisha zoezi la kuwahamisha mpaka pale 
kamati ya kudumu ya huduma za kijamii ya baraza la madiwani 
watakapokutana kutoa maamuzi sahihi juu ya wananchi hao.
Hata
 hivyo agizo hilo la Naibu Waziri limepingwa vikali sana na mkuu wa 
Wilaya ya Singida Mwalimu Qeen Mlozi kwamba Nyalandu hana mamlaka 
kisheria ya kusitisha zoezi hilo, na kwamba anayeweza kumwamuru 
kusitisha zoezi ni Mkuu wa Mkoa pekee na si vinginevyo.
Na Mo Blog 
0 comments:
Post a Comment