MWENYEKITI wa Kijiji  cha Makunda, Kata ya Kyengege, wilayani Iramba
 kwa kushirikiana na watu wengine  zaidi ya 50 wamevamia na kuchoma moto
 nyumba mbili za wakulima wakipinga kuwa  si wazaliwa wa eneo hilo na 
kujipatia ardhi zaidi ya ekari 285.
  Habari za uhakika kutoka katika eneo la tukio  hilo zinaeleza tukio 
hilo limetokea juzi, saa 8:00 mchana katika mashamba ya  kilimo Kijiji 
cha Makunda.
  Kwa mujibu wa habari  hizo, siku ya tukio watuhumiwa wakiwa na silaha 
za jadi walivamia makazi ya  mkulima mwezao, Esau Talanzia (47) na 
kuchoma moto nyumba yake.
  Pia walichoma magunia  sita ya mahindi, magunia mawili ya alizeti 
godoro moja, fedha taslimu sh  450,000 na vitu vingine vilivyokuwemo, 
vyote vikiwa na thamani ya sh milioni  1.8.
  Pia katika tukio hilo  nyumba moja ya Matayo Kizaberga, mkulima na 
mkazi wa Makunda-Mbugani ilichomwa  moto na vitu vyote vilivyokuwemo 
kuteketea.
  Kamanda wa Polisi wa  Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela, alithibitisha 
kutokea kwa tukio hilo na kwamba  watu 25 akiwamo mwenyekiti wa kijiji 
wanashikiliwa na polisi kuhusiana na tukio  hilo.
  Kamanda Kamwela alisema  chanzo cha tukio hilo ni mgogoro wa mashamba 
ambapo wanakijiji cha Makunda  wanapinga waathirika hao kumiliki ekari 
284 wakati si wazawa wa eneo hilo.
  Alisema watuhumiwa wanatarajiwa kufikishwa  mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika.
Chanzo;Tanzania Daima 
0 comments:
Post a Comment