Mkuu
 wa Wilaya ya Mkalama Mkoani Singida Edward Ole Lenga akizungumza na 
wananchi wa kijiji cha Kinampundu mara baada ya kukabidhiwa Zahanati na 
nyumba mbili za mganga na shirika moja lisilo la kiserikali la 
HAPA,hafla hiyo ilifanyikajuzi kijijini hapo.
 Ni
 Mwakilishi wa shirika la SIMAVI kutoka nchini Uholanzi Lieke Ongering 
akizungumza katika hafla ya kukabidhi mradi wake kwa ushirikiano na 
shirika la HAPA Singida kukamilisha mradi wa ujenzi wa Zahanati na 
nyumba mbili za mganga kijiji cha Kinampundu takribani umbali wa 
kilomita 70 kutoka mjini Singida.
Ni
 mmoja wa kinamama wajawazito akipimwa uzito na mkuu wa Wilaya ya 
Mkalama Ole Lenga mara baada ya kukabidhiwa vifaa vya zahanati hiyo, 
anayeshuhudia kipimo hicho ni mhasibu mkuu wa shirika hilo Noel Makyao.
Mkurugenzi
 wa HAPA Davd Mkanje  (Kulia) kimkabidhi DC wa Mkalama Ole Lenga baadhi 
ya vifaa vya kutolea huduma kwenye Zahanati hiyo wakati wa hafla fupi ya
 makabidhiano ya mradi huo.
Ni
 baadhi ya wageni kutoka Mataifa mbalimbali nje ya nchi wakicheza muziki
 na wananchi wa kijiji cha Kinampundu mara baada ya kukabidhiwa mradi 
huo wa afya ya uzazi wa mama na mtoto.
Mkuu
 wa Wilaya ya Mkalama Ole Lenga, kushoto mwenye suti, mwakilishi wa 
SIMAVI, Lieke, MMkurugenzi wa shirika la HAPA, Davd Mkanje na mhasibu 
mkuu wa shirika hilo Noel Makyao wakifurahia pamoja na wananchi mara 
baada ya kukabidhi mradi huo.
Na Hillary Shoo, MKALAMA.
Mkuu
 wa Wilaya ya Mkalama Mkoani Singida ameonya tabia ya baadhi wananchi 
kuezekea kwenye vyoo vyandarua vya kujikinga na mbu wa malaria.
Onyo
 hilo limetolewa mwishoni mwa wiki iliyopita na Mkuu huyo wa Wilaya, 
Edward ole Lenga wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kinampundu
 muda mfupi baada ya kukabidhiwa Zahanti ya kijiji na shirika la HAPA.
Alisema
 imezuka tabia ya wananchi kutumia vyandarua hivyo kwa matumizi yasiyo 
rasmi ikiwa na pamoja na wengine kuvifanya kama mabanda ya kuhifadhi 
vifaranga vya kuku.
“Hii
 ni aibu, wenzetu wanatupatia vyandarua  ili tusipate malaria, nyie 
mnatumia kuezeka vyoo kwa kweli hii ni aibu kubwa sana na mimi 
nimetembea vijijini na kujionea hili, na kwa kweli atakayekamatwa 
atakiona cha moto.” Alisema Dc Lenga kwa masikitiko.
Aidha
 alisema serikali inatumia fedha nyingi kwa ajili ya kuagizi vyandarua 
hivyo kwa ajili kujikinga na mbu wa malaria huku wananchi wakiziona kana
 kwamba hazina msaada na kuzitumia kama kinga kwenye vyoo.
“Hivi
 chandarua kukiezekwa kwenye choo si mtu unaonekana tu , acheni hii 
tabia chafu, nimeunda kikosi kila kijiji atakayebainika kufanya hivyo 
akamatwe na kuletwa kwangu mimi nitamshughulikia ipasavyo.” Alisisitza 
Ole Lenga.
Katika
 hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya aliwataka wananchi wa Wilaya hiyo 
wanaoishi maeneo ya mijini kuja nyumbani na kujenga nyumba na vyoo bora.
Kwa hisani ya Mo Blog 
0 comments:
Post a Comment