Home » » Singida kujenga machinjio ya kuku wa asili

Singida kujenga machinjio ya kuku wa asili

WILAYA ya Iramba mkoani Singida inatarajia kuanzisha machinjio ya kuku wa asili ifikapo Julai mwakani.
Mkuu wa wilaya  hiyo bwana Yahaya Nawanda amebainisha hayo Mjini Kiomboi wakati akifungua   mafunzo ya siku mbili juu ya ufugaji kuku kisasa na kuanzisha SACCOS ya  wafugaji kuku
Amesema lengo la machinjio hayo ya kisasa yaliyopangwa kujengwa katika mji wa Misigiri ni kuhakikisha  kuwa kuku wanaozalishwa wanaongezwa thamani kwa kuchinjwa na kusindikwa ili kukidhi mahitaji ya soko badala ya kusafirishwa hai kwa adha kubwa na wengine kufa njiani.
Amesema uamuzi  wa kujenga machinjio  hayo  umefikiwa baada ya kubaini kuwa licha ya ufugaji wa kuku wa asili kuwa moja ya shughuli kuu za kiuchumi mkoani  Singida, kumekuwepo na changamoto mbalimbali.
Amesema miongoni mwa changamoto hizo ni  pamoja na ukosefu wa soko la uhakika na bei nzuri,  uhaba wa madawa na vifo  vinavyotokana na magonjwa na mazingira magumu ya usafirishaji.
Amesema kujengwa kwa machinjio hayo na kunzishwa kwa soko la kuku  pamoja na kituo cha kutoa elimu juu ya ufugaji wa kuku kisasa,  vitasaidia kuwaingiza wananchi kufuga kuku kibiashara ili kujikomboa kiuchumi.
 Inakadiriwa  kuwa zaidi ya kuku milioni  mbili wa  asali  wanafugwa  mkoani Singida.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa