ZAIDI  ya
shilingi  bilioni 6.4 zimetumika kwa ajili ya shughuli  za
 matengenezo ya barabara kuu, mkoa na madaraja  katika mkoa wa
 Singida katika kipindi cha kuanzia  Januari hadi  Juni mwaka
huu..
Kaimu
meneja wa wakala wa baraara TANROADS mkoa wa Singida Mhandisi Yohannes Mbegalo,
amebainisha hayo jana wakati akizungumza kwenye kikao cha 35 cha bodi ya
barabara.
Mhanadisi 
Mbegalo amesema  kuwa  fedha hizo zimetumika  kwa  ajili ya
kugharamia  shughuli  za matengenezo ya kawaida kwa upande wa
barabara za lami na changarawe zilizopo  mkoani Singida.
Amebainisha baadhi ya
shughuli zilizofanyika kuwa ni pamoja na  matengenezo ya sehemu korofi,
matengenezo ya vipindi maalum pamoja na matengenezo ya  kawaida na 
kujenga makalvati.
Wakala wa barabara
mkoa wa Singida,unahudumia jumla ya kilomita 1,689.5 za barabara kuu na zile za
mkoa.
Kati ya hizo,kilomita
367.9 ni za lami sawa na aslimia 21.8 na sehemu iliyobaki yenye urefu wa
kilomita 1,321.6 sawa na asilimia 78.3 ni za barabara za changarawe  na
udongo.
0 comments:
Post a Comment