Home » » Bilioni 6.4 zatumika ujenzi wa barabara Singida

Bilioni 6.4 zatumika ujenzi wa barabara Singida


ZAIDI  ya shilingi  bilioni 6.4 zimetumika kwa ajili ya shughuli  za  matengenezo ya barabara kuu, mkoa na madaraja  katika mkoa wa  Singida katika kipindi cha kuanzia  Januari hadi  Juni mwaka huu..

Kaimu meneja wa wakala wa baraara TANROADS mkoa wa Singida Mhandisi Yohannes Mbegalo, amebainisha hayo jana wakati akizungumza kwenye kikao cha 35 cha bodi ya barabara.

Mhanadisi  Mbegalo amesema  kuwa  fedha hizo zimetumika  kwa  ajili ya kugharamia  shughuli  za matengenezo ya kawaida kwa upande wa barabara za lami na changarawe zilizopo  mkoani Singida.

Amebainisha baadhi ya shughuli zilizofanyika kuwa ni pamoja na  matengenezo ya sehemu korofi, matengenezo ya vipindi maalum pamoja na matengenezo ya  kawaida na  kujenga makalvati.

Wakala wa barabara mkoa wa Singida,unahudumia jumla ya kilomita 1,689.5 za barabara kuu na zile za mkoa.

Kati ya hizo,kilomita 367.9 ni za lami sawa na aslimia 21.8 na sehemu iliyobaki yenye urefu wa kilomita 1,321.6 sawa na asilimia 78.3 ni za barabara za changarawe  na udongo.


0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa