Mkuu
 wa wilaya ya Ikungi,Manju Msambya, akizungumza kwenye mahafali ya 48 ya
 shule ya msingi ya Mang’onyi.Wa kwanza kushoto ni meneja mahusiano wa 
kampuni ya madini ya Shanta na anayefuatia ni mwenyekiti wa kamati ya 
shule ya msingi ya Mang’onyi, Andrea Andalu.
Mkuu
 wa wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida,Manju Msambya (wa pili kulia) 
akikata utepe kuzindua choo chenye matundu 40 cha shule ya msingi 
Mang’onyi kilichojengwa na kampuni ya Shanta.Wa kwanza kulia ni afisa 
elimu wilaya ya Ikungi Gerald Kivuyo.Wa kwanza kushoto ni meneja 
mahusinao wa kampuni ya madini ya Shanta,Credo Simbaye na anayefuata ni 
mkuu wa shule ya msingi ya Mang’onyi, Adamu Mwekwa.
Mkuu wa wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida, Manju Msambya akigawa vyeti kwa mmoja wa wahitimu wa darasa la saba wa shule hiyo.
Jengo la ofisi ya kijiji cha Mang’onyi kilichojengwa kwa msaada ya kampuni ya madini ya Shanta.
Jengo
 la kituo cha kisasa cha polisi kata ya Mang’onyi kinachoendelea 
kujengwa kwa msaada ana kampuni ya madini ya Shanta.Anayeonyesha jengo 
hilo la kituo cha polisi,ni meneja Ardhi na Makazi wa kampuni ya madini,
 Elisante Kamuya.
Vyumba vya Choo vilivyojengwa na Kampuni ya madini ya Shanta.
Jengo
 la choo cha shule ya msingi cha zamani cha shule ya msingi Mang’onyi 
wilaya ya Ikungi ambacho hakifai kwa matumizi tena.(Picha na Nathaniel 
Limu).
Na Nathaniel Limu, Mang’onyi 
Kampuni
 ya madini ya Shanta Singida imetumia zaidi ya shilingi 23.6 milioni 
kugharamia ujenzi wa choo cha matundu 40 katika shule ya msingi 
Mang’onyi jimbo la Singida mashariki.
Hayo
 yamesemwa juzi na Meneja Mahusiano wa kampuni ya madini Shanta,Credo 
Simbaye wakati akizungumza kwenye hafla ya makabidhiano ya choo hicho 
iliyofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Mang’onyi.
Amesema
 kwamba uamuzi wa kampuni ya Shanta kutoa msaada huo wa ujenzi wa choo 
ni kuinusuru shule hiyo kufungwa kutokana na kukosa choo.
“Baada
 ya mamlaka husika kutaka kuifunga shule hii kongwe kwa muda usiojulika 
kutokana na kukosa kabisa choo kamati ya shule ilileta ombi kwetu 
tusaidie kuijengea choo cha matundu 40 ili isifungwe na wanafunzi zaidi 
ya elfu moja wakakosa masomo ombi hilo tulilipokea kwa mikono 
miwili”,alisema Simbeya 
Meneja
 Mahusiano huyo amesema pamoja na Shanta bado haijaanza shughuli zake za
 uchimbaji madini iliona upo umuhimu mkubwa kujenga choo kwa shule hiyo 
ili wanafunzi wasikatishe masomo kwa tatizo la choo.
“Unapowekeza 
 katika biashara ya madini au maliasili yo yote ile kimsingi unakuwa 
umekubali pia kuwa mdau wa maendeleo ya wananchi katika eneo 
husikajukumu mojawapo ni kuhakikisha kwamba msukumo wa maendeleo 
yanayotarajiwa unapata nguvu za pamoja”amesema Simbaye.
Aidha
 amesema pia hivi sasa wapo kwenye maandalizi ya kuchimba kisima kirefu 
cha maji kitakachosaidia kupunguza uhaba mkubwa wa maji unaochangia 
wakazi wa kata ya Mang’onyi kuchangia maji na mifugo.
“Kama
 nilivyosema awali kwamba Shanta haijaanza kuchimba madini lakini hilo 
halijazuia kampuni kutoa misaada ili kutatua kero mbalimbali 
zinazowakabili wananchi wa kata ya Mang’onyi.
Simbaye
 amesema kwa sasa wanajenga chumba cha darasa katika shule ya msingi 
Mlumba kituo cha kisasa cha polisi kata ya Mang’onyi,vijana 210 wamepata
 ajira za muda na kampuni imeendelea kutoa magari kwa ajili ya 
kusafirisha wagonjwa kuwapeleka kituo cha afya Ikungi na zahanati ya 
kijiji cha Mwau.
“Wito
 wangu kwa wananchi wa wilaya ya Ikungi na hususan wa kata ya Mang’onyi 
,nawaomba waamini kwamba,mradi wa dhahabu wa Shanta Singida,utakapoanza 
utafungua ukurasa mpya wa maendeleo kwa wilaya ya Ikungi na mkoa wa 
Singida,hivyo hawana budi kuunga mkono”,alisema meneja Simbaye.
chanzo: Mo Blog 
0 comments:
Post a Comment