Home » » SINGIDA YAAGIZA DOZI MPYA CHANJO YA UGONJWA WA KIDERI

SINGIDA YAAGIZA DOZI MPYA CHANJO YA UGONJWA WA KIDERI

WILAYA ya Iramba mkoani Singida imelazimika kuagiza  zaidi ya dozi  laki nne za chanjo ya ugonjwa  wa kideri moja kwa moja toka kiwandani, kwa ajili ya kusambaza  kwa wafugaji wa kuku.
Uamuzi huo umefikiwa baada ya kubainika kuwa dawa na chanjo nyingi zinazonunuliwa na   wananchi kwenye maduka binafsi ya kilimo na mifugo zinakuwa zimechakachuliwa na kusababisha kuku kufa.
Akizungumza kwenye  mafunzo ya ufugaji  bora wa kuku, Mkuu wa Wilaya  hiyo Yahaya Nawanda amesema baada ya kubaini tatizo katika chanjo hizo, wameona  vyema kuagiza moja kwa moja toka  kiwandani zinakotengenezwa na kuzimbaza kwa wananchi  wanaofuga kuku Vijijini.
Bwana Nawanda amesema  tayari  mpango huo umeanza kutekelezwa  na  dozi hizo za chanjo zaidi ya laki nne zinatarajiwa kuwa zimewasili  katika Wilaya ya Iramba kabla  ya mwisho wa mwezi huu.
Ufugaji wa kuku wa asili ni moja shughuli kuu za kiuchumi kwa wananchi wa mkoa wa Singida ambapo inakadriwa kuwa hadi kufikia mwishoni mwa mwaka jana zaidi ya kuu milioni mbili walikuwa wanafugwa.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa