WILAYA ya Iramba mkoani Singida imelazimika
kuagiza  zaidi ya dozi  laki nne za chanjo ya ugonjwa  wa kideri
moja kwa moja toka kiwandani, kwa ajili ya kusambaza  kwa wafugaji wa
kuku.
Uamuzi huo umefikiwa baada ya kubainika kuwa
dawa na chanjo nyingi zinazonunuliwa na   wananchi kwenye maduka
binafsi ya kilimo na mifugo zinakuwa zimechakachuliwa na kusababisha kuku kufa.
Akizungumza kwenye  mafunzo ya
ufugaji  bora wa kuku, Mkuu wa Wilaya  hiyo Yahaya Nawanda amesema
baada ya kubaini tatizo katika chanjo hizo, wameona  vyema kuagiza moja
kwa moja toka  kiwandani zinakotengenezwa na kuzimbaza kwa wananchi 
wanaofuga kuku Vijijini.
Bwana Nawanda amesema  tayari  mpango
huo umeanza kutekelezwa  na  dozi hizo za chanjo zaidi ya laki nne
zinatarajiwa kuwa zimewasili  katika Wilaya ya Iramba kabla  ya
mwisho wa mwezi huu.
Ufugaji wa kuku wa asili ni moja shughuli kuu za
kiuchumi kwa wananchi wa mkoa wa Singida ambapo inakadriwa kuwa hadi kufikia
mwishoni mwa mwaka jana zaidi ya kuu milioni mbili walikuwa wanafugwa.
0 comments:
Post a Comment