"FANYENI KAZI KWA BIDII KWA MAENDELEO YA TAIFA" DAS PETER MASINDI

Katibu Tawala wilaya ya Mkalama Ndugu Peter Masindi amewataka watumishi wilayani Mkalama kuwa wazalendo na kufanya kazi kwa bidi katika kuwaenzi mashujaa wa nchi waliopigana kwa ajili ya taifa la Tanzania.
Kauli hiyo ametoa Julai 25, 2024 kwa niaba ya Mkuu wa wilaya ya Mkalama wakati wa zoezi la usafi liliofanyika katika hosipitali ya wilaya ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya Mashujaa nchini.
Serikali inaleta fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miradi, tuwajibike pamoja katika kuhakikisha fedha hizi zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa. Kila mmoja katika nafasi yake atimize wajibu wake, huwezi kuwa shujaa kama ukishindwa kutimiza wajibu wako, kwa kufanya hivi tutakuwa tumewaenzi Mashujaa wetu” DAS Masindi.
Katibu Tawala Peter Masindi amewasisitizia watumishi kuwahudumia wananchi kwa kutumia lugha nzuri pindi wanapokuwa wanatoa huduma kwa wananchi, kulinda maadili ya kazi pamoja na kudumisha amani na umoja baina yao “Tuache ubabe, tuache ufalme kwa kutumia ofisi zetu za serikali, bali tuwatumikie watanzania kwa lugha nzuri” DAS Masindi
Aidha Katibu Tawala Ndugu Peter Masindi amekumbusha watumishi na wananchi wilayani Mkalama kuhusu suala la kulinda maadili ya nchi yetu kwa kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia, vitendo vya ulawati na ushoga katika jamii zetu
“Ndugu zangu Tuhakikishe maadili ya watoto wetu yanajengwa na sisi wazazi, yanajengwa na sisi jamii iliyopo leo, tuhahitaji jamii yenye utuvuli , amani kwa ajili kufikia maendeleo ya taifa letu,hakikisha mtoto anaenda shule, huo ndio Ushujaa unaostahili” DAS Masindi

 

“WAZAZI TUNA WAJIBU WA KUMLINDA MTOTO WAKIKE” DC MACHALI


Mkuu wa wilaya ya Mkalama Mhe. Moses Machali amefanya ziara ya kikazi kwa ajili ya kusikiliza na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wa Kijiji cha Nkinto kilichopo kata ya Nkito wilayani Mkalama.

Akizungumza wakati wa mkutano wa hadhara, Leo Julai 29,2024 Mhe. Machali amewataka wazazi wa Kijiji cha Nkinto na wilayani Mkalama kwa ujumla kuwa mstari wa mbele kupinga mimba za utotoni hasa kwa wanafunzi.

“Tunawajibu mkubwa wa kumlinda mtoto wakike, wananchi wenzangu tushirikiane pamoja kupambana dhidi ya tatizo la mimba mashuleni. Nawaomba sana mtoe ushirikiano pindi kesi za mimba zinapofika Mahakamani, wanaume achaneni na wanafunzi” Mhe. Machali

Mhe. Machali amesisitiza kuwa mzazi yeyote atayebainika kuwa chanzo cha kukwamisha Ushahidi mahakamani atachukuliwa hatua za kisheria “Mtendaji kuanzia leo ikiwa kuna mzazi anahusika nayeye achukulie hatua za kisheria” Mhe. Machali

Akijibu swali kuhusu changamoto ya maji iliyoibuka wakati wa mkutano huo wa hadhara, Mhe. Machali amesema tayari serikali imeshatenga fedha kwa ajili ya kuleta maji safi na hata wataalamu kutoka Mamlaka ya Bonde la Maji mkoa wa Singida wapo Kijiji Nkinto kufuatilia vyanzo vya maji.

“Niwahikishishie wananchi wa Kijiji cha Nkinto na vijiji vya Jirani kuwa tayari watalaamu wetu wako kazini nimeambatanao hapa, mwaka huu hautaisha mtakuwa mmepata Maji” Mhe. Moses Mahali

MHE. JAMES MKWEGA AZINDUA ZAHANATI YA IGENGU


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Mhe. James Mkwega amezindua zahanati ya Igengu ikiwa ni mpango wa serikali wa kuhakikisha kila Kijiji nchini kinakuwa na zahanati.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa zahanati hiyo Julai 20,2024 katika Kijiji cha Igengu, Mhe. James Mkwega ameishukuru serikali pamoja na kwataka wananchi wa Kijiji hicho kulinda afya zao.
 
“Serikali imefanya kazi kubwa, Rais Dkt. Samia kaleta Zahanati na kaleta Umeme. Nampongeza pia Mganga Mkuu wetu Dkt. Solomon Michael kwa kazi kubwa anayofanya lakini pia niwapongeze wananchi kwa kazi kubwa mliofanya. Niwasihi tulinde afya zetu, tuzingatie ushauri wa wataalamu wetu”Mhe. Mkwega
 
Akizungumza kwa niaba ya Mkuregenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Dkt. Solomon Michael amewataka wajawazito wa Igengu kufika kliniki mapema ili kuepusha madhara yanayoweza jitokeza wakati wa kujifungua.
Awali akisoma taarifa kuhusu ujenzi wa zahanati hiyo, Mtendaji wa kata ya Ibaga Ndugu Abdallah Mohamedi amesema zahanati hiyo imegharimu kiasi cha shilingi milioni 110 ikiwa ni fedha kutoka Serikali Kuu, Fedha za Jimbo pamoja na nguvu za wananchi



 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa