Home » » Mkoa wa Singida wazindua mradi wa pikipiki kwa ajili ya kudhibiti uhalifu

Mkoa wa Singida wazindua mradi wa pikipiki kwa ajili ya kudhibiti uhalifu


 Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Vicent Kone (mwenye suti nyeusi) akisalimiana na baadhi ya  viongozi wa jeshi polisi mkoa wa Singida muda mfupi kabla ya kuzindua mradi wa pikipiki kwa ajili ya wakaguzi wa tarafa mkoani Singida.
 Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Vicent Kone akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa mradi wa pikipki kwa ajili ya ukaguzi wa makosa ya uhalifu katika tarafa za mkoa wa Singida. Kushoto ni Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida Linus Sinzumwa na kushoto ni mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida,Mgana Msindai.
 Baadhi ya askari wa jeshi la polisi mkoa wa Singida wakishuhudia uzinduzi wa mradi wa pikipiki kwa ajili ya ukaguzi wa makosa ya uhalifu katika tarafa za mkoa wa Singida.
 Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Vicent Kone akijaribu kuendesha pikipiki za mradi wa ukaguzi wa makosa ya uhalifu katika tarafa za mkoa wa Singida. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singid Mgana Msindai akishuhudia tukio hilo.
Baadhi ya pikipiki 22 za mradi wa ukaguzi wa makosa ya uhalifu katika tarafa za mkoa wa Singida. Pikipiki hizo zimetolewa rasmi kwa ajili ya kukabidhiwa maafisa polisi wa tarafa za mkoa wa Singida.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa