Home » » Wakulima wilaya ya Singida watakiwa kuhakikisha wanaweka akiba ya chakula pindi wanapovuna mazao yao.

Wakulima wilaya ya Singida watakiwa kuhakikisha wanaweka akiba ya chakula pindi wanapovuna mazao yao.

MLOZI 2
Mkuu wa wilaya ya Singida mwalimu Queen Mlozi, ameiagiza idara ya kilimo na mifugo kuangalia uwezekano wa kuanzisha siku maalumu ya sherehe za wakulima ngazi za kata ili pamoja na mambo mengine, wakulima wengi zaidi waweze kutumia fursa hiyo kujifunza kilimo bora.
Mlozi ametoa changamoto hiyo wakati akizungumza kwenye kilele cha sherehe za wakulima wa halmashauri ya wilaya ya Singida zilizofanyika katika kijiji cha Masweya tarafa ya Ilongero.
Amesema utamaduni wa kuendelea kufanya sherehe za wakulima mjini Dodoma kunawanyima fursa wakulima wengi na hasa wadogo kuonyesha mazao yao na pia kujifunza mbinu bora za kilimo.
Mlozi amefafanua kuwa, kama tutasogeza maonyesho ya wakulima hadi ngazi ya kata, faida zake ni nyingi mno kuliko kufanyia mahali ambapo wakulima wetu wengi hawawezi kufika. Faida mojawapo ni kwamba wakulima watajifunza mbinu bora za kilimo na kwa njia hiyo, malengo ya kilimo kwanza, yatafikiwa.
Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya Mlozi amewataka wakulima kutumia vizuri mazao watakayovuna msimu huu na kuhakikisaha wanaweka chakula cha kutosha familia kwa kipindi chote cha mwaka.

CHANZO : MO BLOG

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa