Home » » MWANAMKE AFUNGWA MIAKA 3 KWA KOSA LA KUMNG'ATA MUMEWE SEHEMU ZA SIRI HUKO IRAMBA SINGIDA

MWANAMKE AFUNGWA MIAKA 3 KWA KOSA LA KUMNG'ATA MUMEWE SEHEMU ZA SIRI HUKO IRAMBA SINGIDA







MAHAKAMA ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida 
umemhukumu mwanamke mmoja mkazi wa kijiji
 cha Kisana wilayani humo, Sayuni Ramadhani (42)
 kwenda jela miaka mitatu baada ya kukiri kosa la 
kumng’ata mumewe sehemu zake za siri.Mwendesha 
mashitaka mkaguzi wa polisi, Vincent Ndasa alidai mbele 
ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Iramba,
 Kariho Mrisho kuwa Juni 4 mwaka huu saa 12.00 jioni
 katika kijiji cha Kisana, mshitakiwa kwa makusudi 
alizing’ata kwa meno sehemu za siri za mume wake, 
Onesmo Nathania (42) na kumsababishia maumivu.

Ndasa alidai kuwa siku ya tukio, wanandoa hao 
waliporejea nyumbani kutoka kwenye klabu cha 
pombe ya kienyeji kijijini hao, kulitokea kutokuelewana
 na hivyo kuanza kugombana.Alidai wakati wanaendelea 
kupigana, Onesmo alizidiwa nguvu na kuangushwa chini
 na mkewe ambaye alifungua zipu ya suruali na kufanikiwa 
kuzitoa sehemu za siri za mumewe na 
kuzing'ata nusura azitenganishe.
Mwendesha mashitaka aliendelea kudai
 kuwa mlalamikaji Onesmo alipiga yowe na 
majirani walifika mara moja na kumkimbiza
 katika zahanati ya kijiji kwa ajili ya matibabu.


Mshitakiwa alipoulizwa iwapo ni kweli alikiri 
kosa na akaiomba mahakama imwonee huruma
 kwa kumpa adhabu ndogo kwa kuwa hilo lilikuwa
 ni kosa lake la kwanza na kwamba anahitaji kuwa 
na mumewe ili waendelee kulea idadi 
kubwa ya watoto wao kwa pamoja.
Naye mwendesha mashitaka, Ndasa aliiomba
 mahakama kumpa adhabu kali mshitakiwa
 ili kuwa fundisho kwake na pia kuogofya wanawake 
wanaotarajia kuwafanyia unyama wa aina hii ya
 kung’ata sehemu nyeti za waume zao.
Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mfawidhi Mrisho,
 alisema mahakama yake imezingatia kwa makini 
maombolezo ya mshitakiwa na kufikia uamuzi wa
 kutoa adhabu ya kutumikia jela miaka mitatu.











0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa