Makuli
 kumi wakipakia juu ya lori gunia moja la viazi vitamu lenye zaidi ya 
kilo 150 lenye thamani ya shilingi 35,000.Wakulima wa zao la viazi 
vitamu tarafa ya Ihanja wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida,wamelalamikia 
ujazo huo pamoja na bei wanayopewa kwa madai kuwa ni ya kinyonyaji.
Magunia
 ya zao la viazi vitamu katika kijiji cha Ighuka wilaya ya Ikungi,vikiwa
 tayari kusafirishwa ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kwenda kuuzwa.
Lori
 ambalo dereva wake aliomba lisitajwe namba zake za usajili likiwa 
linapakia magunia ya viazi vitamu katika kijiji cha Ighuka wilaya ya 
Ikungi.(Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel  Limu.
Wakulima
 wa zao la viazi vitamu tarafa ya Ihanja wilaya ya Ikungi mkoani Singida
 wamelalamikia tabia ya wafanyabiashara ya kuwalazimisha kuuza gunia 
lenye uzito wa kilo zaidi ya 150 kwa bei ndogo ya shilingi 35,000.
 Wamedai kwamba ujazo huo wa gunia la viazi vitamu unaojulikana kwa jina la ‘polo’, unachangia wakulima kunyonywa mapato yao.
 Wakizungumza
 kwa nyakati tofauti na MO Blog, wakulima hao wamedai kuwa gharama 
wanazotumia katika kulima na ile ya kusafirisha hadi barabarani zao la 
viazi vitamu, haiwezi kurudi kwa bei wanayopewa na wafanyabiashara hao.
Mmoja
 wa wakulima hao Doricus Hussein, amesema wafanyabiashara hao wanaotoka 
katika mikoa ya Dodoma, Tanga, Dar-es-salaam, Zanzibar pamoja na visiwa 
vya Comoro, wamekuwa hawako tayari kununua zao hilo kwa kutumia vipimo 
kwa madai kuwa hakuna soko litakalonunua viazi vitamu kwa kutumia 
mizani.
 Alitumia
 fursa hiyo kuiomba serikali ya kijiji kwa ushirikiano na halmashauri ya
 wilaya ya Ikungi,kuangalia uwezekano wa kuwasaidia wakulima wasiendelee
 kunyanyaswa na kudhulumiwa na wafanyabiashara hao.
 Kwa
 upande wake Kaimu Afisa Mtendaji wa kata ya Pum Miraji Ntungu, amesema 
kuwa licha ya kupiga marufuku ujazo wa rumbesa unaolalamikiwa na 
wakulima hao, lakini ni wakulima wenyewe ndio wanaopingana na agizo hilo
 kwa madai kuwa serikali haijawasaidia kutafuta mbegu ya viazi vitamu.
 Ntungu
 amesema kwa siku moja magunia yasiyopungua 200 husafirishwa kutoka 
kijiji cha Puma pekee kwenda kwenye masoko ya ndani na nje ya nchi, 
ambapo kila gunia hulipiwa ushuru wa shilingi elfu moja.
 Kwa
 upande wao wafanyabiashara hao wanaolalamikiwa, wamedai kuwa hakuna 
soko linaloweza kununua gunia la viazi vitamu  lisilo kuwa na ujazo wa 
rumbesa iliyopitiliza.
 Mmoja
 wa wafanyabiashara hao Bw. Shabani Hamisi Bilali, amesema pia 
wanawataka wakulima hao kujaza gunia ujazo huo wa rumbesa ili pamoja na 
mambo mengine, wao waweze kufidia gharama za upakiaji na  usafirishaji  
na hivyo kupata faida inayokidhi mahitaji.
 Na Mo Blog
0 comments:
Post a Comment