Mkuu
 wa wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Gishuli Charles (kulia) akitoa 
maelekezo juu ya mikakati ya kuboresha kilimo cha pamba mbele ya wajumbe
 wa kikao cha kazi cha kutathimini zao la pamba msimu huu 
kilichohudhuriwa na wajumbe kutoka bodi ya pamba na wadau wa zao hilo. 
Dc Charles alikuwa mwenyekiti wa kikao hicho kilichofanyika kwenye 
ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa mjini hapa. Kushoto ni kaimu
 katibu tawala mkoa wa Singida,Mumba.
Baadhi
 ya wajumbe wa kikao cha kazi cha kutathimini kilimo cha pamba cha msimu
 huu kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa 
mjini Singida.(Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
MVUA
 zilizonyesha kwa mtawanyiko usioridhisha msimu huu na kusababisha ukame
 mkali,zimeathiri zaidi ya hekta 2,000 za zao la pamba na mavuno 
yanatarajiwa kuwa hafifu;imeelezwa.
Hayo
 yamesemwa na mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone,wakati akifungua 
kikao cha kazi cha wadau wa zao la pamba mkoani hapa, kilichofanyika 
kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa mjini hapa.
Alisema
 kwa kuzingatia hilo,mkoa wa Singida kwa kushirikiana na bodi ya pamba 
umeona umuhimu wa kukutanisha wadau wa zao la pamba ili kujadili 
maendeleo ya kilimo cha pamba cha mkataba ambacho kina tija zaidi.
Aidha,
 Dk.Kone alisema kukutana huko pia zitatolewa taarifa  za mafanikio na 
changamoto mbalimbali zilizojitokeza msimu wa 2014/2015,na kuweka 
mikakati ya kufanikisha masuala ya soko la pamba katika msimu huu.
“Napenda
 tuelewe kuwa mkutano huu ni fursa nzuri ya kuwakutanisha viongozi na 
wataalam wa ngazi ya wizara,mkoa,halmashauri na wakulima,ili kujadiliana
 mafanikio yaliyopatikana,changamoto zilizopo na kuweka mikakati ya 
kuhakikisha juhudi za kuongeza tija na faida katika uzalishaji wa zao la
 pamba, zinaendelezwa”,alifafanua.
Katika
 hatua nyingine,Dk.Kone alisema katika msimu huu jumla ya wakulima 821 
wa zao la pamba,wamepewa mafunzo ya kilimo bora cha pamba.
Aidha,
 alisema katika msimu huu jumla ya hekta 6,757 za pamba zimelimwa,chupa 
11,346 za viuatilifu na mabomba 35 ya kunyunyizia pamba,yalisambazwa na 
kampuni pekee inayoshughulkia zao la pamba mkoani hapa ya Biosustain ya 
jijini Dar-es-salaam.
“Nitumie
 fursa hii kuipongeza kampuni ya Biosustain kwa kazi nzuri 
inayojishughulisha na kilimo cha mkataba mkoani mwetu.Kampuni hii 
imeweza kufufua zao la pamba kwa kuanzisha kiwanda cha kuchambua 
pamba.Mfumo wa kilimo cha mkataba umeweza kunufaisha wakulima 
2,500”,alisema Dk.Kone.
Zao
 la pamba ni miongoni mwa mazao makuu manne ya biashara yanayozalishwa 
hapa nchini na linachukua nafasi ya nne kwa kuchangia uchumi wa 
taifa.Wastani wa faifa wa uzalishaji, ni kilo 300 kwa ekari 
ikilinganishwa na lengo lililowekwa la kufikia uzalishaji wa kilo 1,500 
kwa ekari ifikapo mwaka huu wa 2015.
Kwa
 mkoa wa Singida,hali ya uzalishaji wa pamba imekuwa ikibadilika kwa 
kiasi kikubwa ikilinganishwa na mazao mengine ya biashara, kutokana na 
kuyumba kwa bei ya zao hilo mwaka hadi mwaka.
Baadhi
 ya mikakati ya kuimarisha kilimo cha pamba mkoani hapa ambayo imewekwa 
na kikao hicho,ni pamoja na kuhamasisha kila kaya inalima si chini ya 
ekari mbili kila msimu.
Mikakati
 mingine ni halmashauri kushirikiana na wataalamu wa vipimo kuhakikisha 
matumizi sahihi ya vipimo yanatumika wakati wa kuuza pamba,kuhimiza 
kilimo cha mkataba na kila mdau wa kilimo cha pamba,atimize wajibu wake.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
0 comments:
Post a Comment