Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mbunge
 wa viti maalum mkoa wa Singida, Martha Mosses Mlata, akishiriki 
kutekeleza agizo ya rais Dk. John Pombe Magufuli la Watanzania wote 
kufanya usafi katika maeneo yao, kama sehemu ya maadhimisho ya sherehe 
za Uhuru kutimiza miaka 54, kwa kufanya usafi kwenye chuo cha wasioona 
cha mjini hapa. Pamoja na kufanya usafi chuoni hapo, Mlata alitoa msaada
 wa vifaa mbalimbali ikiwemo viti vya plastiki 150.Thamani ya msaada 
huo, ni zaidi ya shilingi 6.3  milioni.
Mbunge
 wa viti maalum mkoani Singida, Martha Mosses Mlata, akikabidhi msaada 
wa vifaa mbalimbali wenye thamani ya zaidi ya shilingi 6.3 milioni kwa 
uongozi wa Chuo cha wasioona cha mjini hapa. Msaada huo ni sehemu ya 
maadhimisho ya sherehe za Uhuru kutimiza miaka 54.(Picha na Nathaniel 
Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
MBUNGE
 wa viti maalum (CCM) mkoani Singida,Martha Mosses Mlata, (9/12/2015) 
ametumia zaidi ya saa tatu kufanya usafi katika Chuo cha Watu Wasioona 
kilichopo Manispaa ya Singida.
Mlata
 ambaye alifuatana na baadhi ya wana CCM wa Manispaa ya Singida, 
alifanya usafi huo ikiwa ni kutekeleza agizo la Rais Dk.John Pombe 
Magufuli kama sehemu ya maadhimisho ya sherehe za kutimiza miaka 54 ya 
Uhuru.
Mbunge
 huyo alisema kuwa anamuuga mkono Rais Magufuli kwa kuhimiza usafi wa 
mazingira kitendo ambacho pamoja na mambo mengine,kitapunguza uwezekano 
wa kutokea kwa magonjwa ya mlipuko ukiwemo kipindupindu
“Tabia
 hii ya kufanya usafi kwenye maeneo yatu na yale mengineyo, inapaswa iwe
 endelevu kutokana na faida zake kuwa nyingi.Pia mazingira yakiwa 
masafi,yanapelekea kuvutia zaidi”,alisema mbunge Mlata.
Pamoja
 na kufanya usafi sehemu mbalimbali za chuo hicho ikiwemo maeneo ya 
vyoo,Mlata alitoa msaada wa vifaa mbalimbali vikiwemo vya kufanyia 
usafi, viti 150 vya plastiki na mazulia.Vifaa hivyo vina thamani ya 
zaidi ya shilingi 6.3 milioni.
0 comments:
Post a Comment