Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida, ACP.Thobias Sedoyeka.
Na Nathaniel Limu, Singida-Mo Blog
Jeshi
 la polisi mkoani Singida,limefanikiwa kukamata mkulima na mkazi wa 
Kibaoni Iddy Issah (33), anayedhaniwa kuwa ni  jambazi sugu baada ya 
kulipiga risasi moja mguu wake wa kulia, wakati alipojaribu kutoroka.
Kaimu
 kamanda wa polisi mkoa wa Singida, ACP Simon Haule,alisema mtuhumiwa 
huyo amekamatwa Januari tatu mwaka huu saa 7.20 usiku katika baa ya 
Leaders iliyopo kata ya Kindai tarafa ya Unyakumi manispaa ya Singida.
Alisema
 siku ya tukio askari polisi walipokuwa kwenye doria katika mitaa ya 
kata ya Kindai, walipata taarifa za kiintelijensia kuwa mtuhumiwa yupo 
baa ya Leaders maeneo ya Kibaoni.
“Baada
 ya polisi hao kupata taarifa hizo,walifika haraka kwenye baa hiyo na 
kujaribu kumkamata mtuhumiwa.Lakini alipambana nao huku akitaka 
kumnyang’anya silaha mmoja wa askari polisi hao,hata hivyo,hakuweza 
kufanikiwa”,alisema Haule.
Kaimu
 kamanda huyo,alisema baada mtuhumiwa kushindwa kupora silaha,  
alifanikiwa kukimbia akitaka kutoroka ndipo  askari mmoja alifyetua 
risasi mbili hewani, ili kumwongofya aweze kusimama.Hakuweza 
kusimama,kitendo kilichomlazimisha askari kumjeruhi mguu wa kulia.
Kuhusu
 tuhuma zinazomkabili mtuhumiwa, Haule alisema  amefunguliwa kesi 
SI/IR/4412/2015 ya kuvunja nyumba usiku na kumwimbia  raia wa kigeni 
kutoka China, shilingi 17,442,000.
“Mwaka
 jana pia alifunguliwa kesi no.SI/1R/4722/2015 ya kuvunja nyumba usiku 
na kuiba shilingi 200,000 mali ya raia wa kigeni kutoka Korea. Ana kesi 
nyingine no.SI/1R/4723/2015 ya kuvunja nyumba usiku na kuiba fedha na 
simu  vyote vikiwa na thamani shilingi 3,101,000.Makosa hayo yote 
yanaangukia chini ya kifungu cha sheria namba 294 (2) na 296 (a) vya 
kanuni ya adhabu”, alifafanua.
Alisema
 kwa sasa mtuhumiwa Iddy amelazwa wodi namba tatu katika hospitali ya 
mkoa mjini hapa chini ya ulinzi mkali, na hali yake inaendelea vizuri.
Haule alisema baada ya upelelezi zaidi kukamilika,mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma inayomkabili.
0 comments:
Post a Comment