Mkuu
 wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone, akifungua hafla ya uzinduzi wa bodi
 ya maji bonde la kati. Hafla hiyo ilifanyika kwenye ukumbi wa mikutano 
wa Aqua Resort Vitae mjini hapa. Kulia ni Mwenyekiti  mpya wa bodi ya 
maji bonde la kati, Eng.Samson Babala na kushoto ni Naibu Katibu 
TAMISEMI, Eng.Emmanuel Kalobelo.
Naibu
 Katibu Mkuu TAMISEMI, Eng.Emmanuel Kalobelo, akitoa nasaha zake kwenye 
hafla ya uzinduzi wa bodi mpya ya maji bonde la kati uliyofanyika kwenye
 ukumbi wa mikutano wa Aqua Resort Vitae mjini hapa. Wa kwanza kulia ni 
Mwenyekiti mpya wa bodi ya maji bonde la kati, Eng.Samson Babala, wa 
pili kulia ni Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone na kushoto ni 
Mwenyekiti mstaafu bodi ya maji bonde la kati, Eng.Mwanaasha Ally.
Mwenyekiti
 mstaafu wa bodi ya maji bonde la kati, Eng.Mwanaasha Ally, akitoa 
nasaha zake kwenye hafla ya uzinduzi wa bodi mpya ya maji bonde la kati 
iliyofanyika mjini hapa jana.Kushoto walioketi  ni Naibu Katibu Mkuu 
TAMISEMI, Eng.Emmanuel Kalobelo, katikati ni Mkuu wa mkoa wa Singida, 
Dk.Parseko Kone na wa kwanza kulia ni Mwenyekiti mpya bodi ya maji bonde
 la kati, Eng.Samson Babala.
Baadhi
 ya wajumbe wa bodi ya maji bonde la kati waliohudhuria hafla ya 
uzinduzi bodi hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Aqua resort
 vitae mjini hapa.(Picha na .Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
MKUU
 wa mkoa wa Singida, ameuhimiza uongozi mya wa bodi ya maji bonde la 
kati kufanya maandalizi ya kina yatakayowezesha kupata mbinu na njia za 
kisasa za kusimamia na kugawa maji,ili kuepusha migogoro ya maji.
Dk.Kone
 ametoa rai hiyo wakati akizindua bodi ya nne ya maji bonde la 
kati.Uzinduzi huo ulifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Aqua Vitae 
Hoteli mjini hapa.
Alisema
 Tanzania inalenga kwenda kwenye uchumi wa kati ifikapo mwaka 
2025,mojawapo ya vichocheo vikubwa katika kufikia malengo hayo,ni 
mapinduzi ya kilimo na viwanda ambavyo yatahitaji maji mengi  na ya 
kutosha.
Dk.Kone
 alisema pamoja na kilimo na viwanda kuhitaji maji ya kutosha,pia 
ongezeko la watu na shughuli zao mbalimbali zikiwemo za 
kiuchumi,zinazitaji kiwango kikubwa cha maji.
“Kutokana
 na uhitaji huo mkubwa wa maji,uwezekano wa kutokea kwa migogoro 
itakayotokana na uhitaji wa maji,ni mkubwa.Nina taarifa kuwa tayari 
migogoro hii imeanza kuongezeka hasa katika maeneo ya mikoa ya Manyara 
na Arusha.Bodi hii ni lazima isimamie kikamilifu masuala haya kwa 
ukamilifu na ufanisi mkubwa”,alisema.
Katika
 hatua nyingine,mkuu huyo wa mkoa alisema maamuzi mengi duniani ambayo 
ni pamoja na yanayohusu maji,yanafanywa na wanasiasa au na viongozi 
ambao ni wanasiasa.
“Kwa
 hiyo katika utendaji kazi wenu,hamna budi kushirikiana na wanasiasa na 
viongozi wengine wa serikali katika ngazi za kitaifa,mikoa,wilaya,kata 
na vijiji,ili kutatua changamoto za maji kwa pamoja”,alisema.
Aidha,Dk.Kone
 ametoa rai kwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji, katika bajeti
 ya maji watoe kipaumbele katika utunzaji na usimamizi wa rasilimali za 
maji, ukusanyaji na uchambuzi wa takwimu za maji kwa wingi.
“Bila
 takwimu za muda mrefu na sahihi,usimamizi wa rasilimali za maji utakuwa
 ni mgumu sana na unakuwa sio wa kisayansi”,alifafanua Dk.Kone.
Awali
 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Eng.Emmanuel Kalobelo,
 alisema majukumu ya msingi ya bodi ya maji za mabonde,ni 
kusimamia,kupanga na kuendeleza rasilimali za maji zilizoko katika 
mabonde.
“Bodi
 hizi zikifanya kazi zake vizuri,Watanzania tutakuwa na uhakika wa 
uatikanaji endelevu wa maji,kwani bodi hizi ni lazima zitayarishe miango
 ya usimamizi wa rasilimali za maji katika mabonde.
Akifafannua
 zaidi, Eng.Kalobela,alisema bodi za maji za mabonde zinaaswa 
kushirikiana na wadau wengine kutatua migogoro ya utunzaji wa maji 
inayojitokeza katika maeneo yao.
Kwa
 mujibu wa Naibu Katibu Mkuu huyo, Tanzania ina mabonde tisa, ambayo ni 
bonde la Pangani, Ruvuma, waMi ya kusini, Rufiji, Wawi/Ruvu, Ziwa 
Victoria, Ziwa Nyasa, Ziwa Rukwa, Ziwa Tanganyika na bonde la kati.
Na Mo Blog  
0 comments:
Post a Comment