Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
KATIBU Tawala wa Mkoa wa Singida, Festo Kang’ombe ametaka kuwepo na 
nguvu ya ushawishi katika kupata wanachama wa Mfuko wa Afya ya Jamii 
(CHF) na si kuwalazimisha wananchi na kusababisha wakimbilie porini kwa 
sababu za michango.
Alisema hivyo wakati akifungua mkutano wa siku ya wadau katika 
wilayani hapa, ikiwa ni sehemu ya upitishaji wa mchakato wa kutungwa kwa
 sheria ndogo na kutengenezwa hati kwa lengo la kuwezeshwa kuendeshwa 
kwa mpango wa CHF wilayani humo.
Mchakato huo unaokwenda hatua kwa hatua, unatarajiwa kukamilishwa wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani.
Alisema, pamoja na uzuri wa mpango huo ambao ni wa hiari, wananchi 
wanatakiwa kushawishiwa na si kulazimishwa kwa kutumia mabavu, ili 
wajiunga na CHF.
Kang’ombe alisema, wilaya ya Mkalama si ngeni katika utekelezaji wa 
mpango wa CHF na kwamba muitikio mkubwa utakaowezesha kuimarisha huduma 
za afya wilayani hapo utatokana na nguvu za hoja na wala si hoja za 
nguvu.
Alisema, wilaya hiyo mpya ilikuwa awali ikitekeleza mpango huo chini 
ya wilaya ya Iramba na ilionesha mafanikio makubwa tangu kuanzishwa 
kwake mwaka 2004 ndio maana wilaya nyingi zilifika kujifunza.
Kang’ombe alisema, alipokuwa Ofisa Mipango katika wilaya ya Kahama 
walifika kujifunza uendeshaji wa CHF, safari ambayo pia iliwafikisha 
Igunga na Mbinga.
Alisema, taifa lenye wagonjwa haliwezi kusonga mbele na uwekaji wa 
nguvu za pamoja utawezesha matatizo ya sekta ya afya yaliyopo kwa sasa 
kuondoka.
 CHANZO ; HABARI LEO.
0 comments:
Post a Comment