Mwana
 CCM, Martha Mosses Mlata (kushoto) akirejesha fomu za kugombea nafasi 
ya Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida kwa Katibu msaidizi CCM mkoa wa 
Singida, Adamu Makulilo leo.Nafasi ya Mwenyekiti wa CCM mkoa wa 
Singida,iliachwa wazi na Mgana Izumbe Msindai aliyetimkia CHADEMA baada 
ya kushindwa kwenye kura za maoni wakati wa kinyang’anyiro za kura za 
maoni (nafasi ya ubunge) ndani ya CCM.
Mwanyekiti
 wa jumuiya ya wazazi (CCM) mkoa wa Singida, Yusuph Mwandami Gwayoka 
(kushoto) akikabidhiwa fomu ya kugombea nafasi ya mwenyekiti wa CCM mkoa
 wa Singida na Katibu msaidizi CCM mkoa wa Singida, Adamu Makulilo.Picha
 na Nathaniel Limu.
Na Nathaniel Limu, Singida
MBUNGE
 wa viti maalum (CCM)  mkoa wa  Singida, Martha Mosses Mlata ni miongoni
 mwa wana CCM sita ambao wamejitokeza kuomba kuziba nafasi iliyoachwa 
wazi na Mgana Izumbe Msindai ya mwenyekiti wa CCM mkoa aliyetimkia 
CHADEMA muda mfupi baada ya kushindwa kwenye uchaguzi wa kura za maoni 
(CCM) kugombea ubunge.
Wana
 CCM wengine waliochukua fomu hadi leo jioni toka zoezi la uchukuaji 
fomu lianze Januari sita mwaka huu asubuhi,ni Juma Hassan Kilimba, 
Mohammed Hamisi Missanga, Narumba Barnaba Hanje, Shafii Juma Mtaturu na 
Yusuh Mwandami Gwayoka.
Katibu
 msaidizi wa CCM mkoa wa Singida,Adamu Makulilo,alisema hadi sasa 
aliyekuwa mbunge wa jimbo la Iramba Juma Hassan Kilimba,Martha Mlata na 
aliyemaliza muda wake wa ubunge wa jimbo la Singida magharibi mwaka 
jana,Mohammed Hamisi Missanga,wameisha rejesha fomu zao.
Adamu alisema zoezi hilo la utoaji wa fomu bado linaendelea na linatarajiwa kukoma januari 10 mwaka huu saa kumi jioni.
“Nitumie
 fursa hii kuwaomba wana CCM  wajitokeze kwa wingi na hasa wale 
watakaojipima na kubaini wanao uwezo wa kuvaa viatu vilivyoachwa na 
Mgana Msindai,ili kuleta upinzani wa kweli utakaosaidia CCM kupata 
mwenyekiti atakayemudu kasi iliyopo hivi sasa nchini.Ada ya fomu ni kama
 bure kabisa, kwa sababu tunatoza fomu ‘buku’ tu (shilingi 
10,000)”,alisema katibu msaidizi huyo.
Akizungumza
 na mwandishi wa habari hii kwenye viwanja vya CCM mkoa,Mlata alisema 
kuwa safari hii ni zamu ya mwanamke kuongoza chama tawala mkoani hapa,na
 kwamba mwanamke huyo si mwingine isipokuwa ni yeye (Mlata).
Alisema
 amejikagua na kujitathimini na kubaini kwamba anao uzoefu wa kutosha 
kuwatumikia wana CCM na wananchi kwa ujumla katika nafasi hiyo ya 
mwenyekiti CCM mkoa.
“Kupitia
 nafasi mbalimbali nilizozipata ikiwemo ya ubunge wa viti 
maalum,nafahamu vyema Chama Cha Mainduzi kinavyoongozwa,nazijua 
changamoto ya chama chetu kuanzia ngazi ya chini ya tawi hadi mkoa.Kwa 
ukweli huo,mimi ni chaguo sahihi kupewa nafasi iliyoachwa wazi na kaka 
yangu Msindai”,alisema.
Mlata
 aliyesema endapo atafanikiwa kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa CCM mkoa wa
 Singida,atatumia nguvu zake zote amoja na wanachama wengine,kurejesha 
umoja na mshikamano miongoni mwa wana CCM,ili mkoa uendelee kuwa wa CCM 
chama cheye sera zinazotekelezeka.
“Nitashirikiana
 na wana CCM wenzangu kukiimarisha chama na kuhakikisha CCM inawajengea 
mazingira mazuri wananchama wake ili waweze kuboresha hali zao za 
kiuchumi.Tatizo linalosababisha mwanachama ye yote wa chama cho chote 
cha saisa kuhama hama,ni umaskini tu.Lakini mtu kama ana uwezo mzuri 
kiuchumi,huyo sio rahisi kumurubuni au kumdanganya”,alisema Mlata.
Kwa
 upande wake Yusuph Mwandami Gwayoka, alisema kuitia nafasi yake ya 
mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi mkoa,anayo uzoefu wa kutosha wa kumudu 
nafasi ya mwenyekiti CCM mkoa.
“Mimi
 nimejipanga vema kushindana na wana CCM wenzangu katika kuwania nafasi 
hii ya mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida. Niwaase tu wagombea wenzangu 
kwamba tunakwenda kushindana na wala hatuendi kugombana.Kwa hali 
hiyo,kabla na baada ya matokeo kutangazwa,tuendelee kudumisha umoja na 
mshikamano na ikiwezekana,ushirikiano tulio nao,tuuboreshe 
zaidi”,alifafanua Mwandami.
MO BLOG 
0 comments:
Post a Comment