Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Ni Katibu wa TSD Mkoa wa Singida,Bwana Samweli Ole 
Saitabau(aliyesimama) akitoa ufafanuzi juu ya upatikanaji wa haki za 
walimu wa wilaya ya Manyoni ambao bado haapandishwa madaraja yao.

Ni Baadhi ya wanachama wa CWT Wilaya ya Manyoni,Mkoani Singida wakiwa katika mkutano wa pamoja na Naibu Katibu Muu wa CWT,Bwana Ezekiah Oluoch .
Ni Baadhi ya wanachama wa CWT Wilaya ya Manyoni,Mkoani Singida wakiwa katika mkutano wa pamoja na Naibu Katibu Muu wa CWT,Bwana Ezekiah Oluoch .
WALIMU
 447 wa shule za msingi na sekondari katika Halmashauri ya wilaya ya 
Manyoni,Mkoani Singida hawajapandishwa madaraja yao mbalimbali kutoka 
mwaka 2014/2015 mpaka sasa hali ambayo imepunguza ari ya utendaji wao wa
 kazi za kila siku.
Katibu
 wa Chama Cha Walimu (CWT) Wilaya ya Manyoni, Nelea Nyang’uye aliyasema 
hayo kwenye taarifa ya kamati ya utendaji ya chama hicho aliyotoa kwa 
Naibu katibu mkuu CWT,Ezekiah Oluoch aliyekuwa na ziara ya siku moja 
wilayani Manyoni iliyolenga kusikiliza kero pamoja na kuzitafutia 
ufumbuzi.
Aidha
 Nelea alifafanua kwamba kati ya walimu hao,walimu 390 ni walimu wa 
shule za msingi na kwamba walimu 276 licha ya kuwa na sifa za 
kupandishwa madaraja lakini mpaka wamefikia hatua ya kugota na bila 
kupandishwa na walimu 114 wanastahili kupandishwa kwa utaratibu wa 
kawaida.
Kwa 
mujibu wa katibu huyo wa CWT,kwa upande wa idara ya elimu sekondari kuna
 walimu 9 waliogota na walimu 50 wanastahili kupandishwa kwa utaratibu 
wa kawaida lakini mamlaka zinazohusika zimeshindwa kushughulikia 
wilayani hapa.
Kuhusu
 malipo ya fedha za likizo,Nyang’uye aliweka bayana kuwa kwa kipindi cha
 mwezi disemba,mwaka jana Halmashauri ya wilaya ya Manyoni ilitarajia 
kupokea shilingi milioni 30 lakini fedha walizopokea ni shilingi milioni
 21 na hivyo kuwa na upungufu wa shilingi milioni saba.
Hata
 hivyo msemaji huyo wa chama alisisitiza kwamba fedha hizo za nauli ya 
likizo hupelekwa kidogo sana na kibaya zaidi fedha hizo hupelekwa wakati
 likizo ikiwa imeshaanza au inakaribia kwisha,jambo ambalo linapelekea 
walimu wwenye haki ya kulipwa kuanza kukopa.
“Nauli
 za likizo kuletwa kidogo mno na zinaletwa wakati likizo ikiwa imeanza 
au inakaribia kwisha,jambo ambalo linapelekea walimu wenye haki ya 
kulipwa kuanza kukopa,kwa mfano nauli ya mwezi disemba,mwaka jana 
iliyoletwa kwa idara ya elimu ya msingi ni shilingi 23,000,000/= na 
idara ya elimu sekondari ni shilingi milioni saba”alisisitiza katibu 
huyo wa CWT.
Nyang’uye
 hata hivyo alionyesha masikitiko yake kutokana na Tume ya Utumishi wa 
Walimu(TSD) wilaya ya Manyoni kushindwa kushughulikia mashauri ya 
kinidhamu kwa wakati na hivyo kuchukua muda mrefu sana na kutoa mfano wa
 shauri moja la walimu wawili waliosimamishwa kazi tangu mwaka 2013 
mpaka sasa hawajuia hatma yao.
Picha na Michuzi Media 
0 comments:
Post a Comment