Home » » Kukosekana kwa Daraja katika Mto Saiwa wa kijiji cha Minyughe, kwawa kero kwa wananchi

Kukosekana kwa Daraja katika Mto Saiwa wa kijiji cha Minyughe, kwawa kero kwa wananchi

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

IMG_0654
Diwani mteule (CCM) kata ya Minyughe (wa tatu kushoto mwenye suti ya bluu) Samweli Daniel Sadiki, pamoja na wakazi wa kijiji cha Minyughe,wakiangalia gari aina ya fuso T.662 CBB la kampuni ya Pepsi lililosombwa na maji ya mvua katika mto Saiwa.
IMG_0664
Gari aina na fuso T.662 CBB  la kampuni ya Pepsi mjini Singida, likiwa limeangushwa na kusombwa na maji ya mvua katika mto Saiwa wa kijiji cha Minyughe wilaya ya Ikungi. Gari lililokuwa linasambaza soda katika vijiji vya kata ya Minyughe lipo mtoni hapo kwa zaidi ya wiki moja,baada ya kushindikana kutolewa mtoni hapo. Hali hiyo imesababishwa na mto huo kutokuwa na daraja hali inayochangia pia kuhatarisha maisha ya wananchi na mali zao.
IMG_0663
Baadhi ya wakazi wa kata ya Minyughe tarafa ya Ihanja,wakivuka mto Saiwa ambao unadaiwa kutokuwa na daraja, jambo ambalo ni hatari kwa wananchi na mali zao.
IMG_0680
IMG_0676
Landrover 110 likiwa limekwama kwenye mto Saiwa kutokana na mchanga wa mto huo kujaa maji na kusababisha magari kukwama.Hali hiyo inachangiwa na mto huo mkubwa kutokuwa na daraja.
IMG_0682
Wakazi wa kata ya Minyughe wakisaidiana kuvuka mto Saiwa baada ya maji ya mvua kupungua.Imedaiwa kuwa mto huo ambao hufurika maji wakati mvua zinaponyesha,hauna daraja hali inayohatarisha maisha ya watu na mali zao.Hata hivyo,mhandisi wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi mkoani Singida, injinia Haruna Mbagalla,amesema ujenzi wa daraja katika mto huo,unatajariwa kuanza mapema januari mwakani.(Picha zote na Nathaniel Limu).

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa