Home » » SHULE YA SEKONDARI MWENGE YADAIWA MILIONI 396

SHULE YA SEKONDARI MWENGE YADAIWA MILIONI 396

 SHULE  ya  Sekondari ya  Mwenge  ya Mjini Singida  ambayo  hivi sasa inachukuwa wanafunzi wa  kidato  cha tano na sita  pekee, inadaiwa zaidi ya shilingi milioni 396.6 na wazabuni waliofanya manunuzi na kutoa  huduma  mbalimbali katika kipindi cha miaka kumi iliyopita.

Mkuu wa Wilaya ya Singida bibi Queen Mlozi amebainisha hayo  jana wakati akitoa taarifa yake kwa mkuu wa mkoa wa Singida Dokta Parseko Kone aliyefanya ziara ya kikazi ya siku moja katika  halmashauri ya Manispaa ya Singida ilipo shule hiyo kongwe nchini.

Amesema kati ya fedha hizo, shilingi milioni 357.6, ni madeni mbalimbali ya wazabuni waliotoa  chakula  na huduma  nyingine muhimu katika shule hiyo kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita.


Bibi Mlozi amesema kiasi kingine cha zaidi ya shilingi milioni 38.9, ni madeni  ya dawa na vifaa mbalimbali vilivyotumika  kufanyia majaribio maabara katika shule hiyo tangu 2008 hadi mwaka jana.

Amesema deni hilo ni kikwazo  kikubwa kwa ustawi na maendeleo ya shule hiyo kutokana na  kushindwa kuamikika tena na wazabuni ili iendelee kupatiwa huduma mbalimbali.

Mkuu wa mkoa wa Singida Dokta Parseko Kone ameahidi kuunganisha nguvu na mamlaka zingine  kulitafutia ufumbuzi suala hilo.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa