KAMPUNI
ya simu  nchini  (TTCL) mkoani Singida inadai  zaidi ya shilingi
 milioni 524.6 zikiwa ni malimbikizo ya ankra za matumizi ya simu kwa
wateja wake  katika kipindi  cha  kuanzia mwaka juzi hadi machi
mwaka huu.
Meneja
biashara wa Kampuni hiyo ya TTCL  mkoa wa Singida bw Mwindadi Baule,
amesema hayo wakati wa chakula cha mchana walichokiandaa kwa wafanyabiashara
wakubwa wa mjini Singida. 
Lengo
la  chakula hicho pamoja na kuimarisha mahusiano baina ya  Kampuni na
wateja wake, ni kuwaelimisha wafanyabiashara  hao kulipa madenbi yao kwa
wakati ili kuiwezesha Kampuni  kujiendesha na kuboresha huduma.
Amesema
 kutolipwa kwa wakati kwa deni  hilo  ni moja  ya sababu
zinazoleta changamoto kubwa katika kuboresha  huduma kwa wateja pamoja na
kusambaza zaidi  huduma hiyo hadi  Vijijini.
Hata 
hivyo amesema mikakati mbalimbali  imewekwa na kampuni hiyo ikiwemo
kutumia vyombo  vya kisheria kwa ajili ya kuhakikisha kuwa kila mteja
anayedaiwa analipa deni lake  mara moja.
0 comments:
Post a Comment