Home » » TTCL SINGIDA YADAI MIL.524 KUTOKA KWA WATEJA WAKE

TTCL SINGIDA YADAI MIL.524 KUTOKA KWA WATEJA WAKE

KAMPUNI ya simu  nchini  (TTCL) mkoani Singida inadai  zaidi ya shilingi  milioni 524.6 zikiwa ni malimbikizo ya ankra za matumizi ya simu kwa wateja wake  katika kipindi  cha  kuanzia mwaka juzi hadi machi mwaka huu.

Meneja biashara wa Kampuni hiyo ya TTCL  mkoa wa Singida bw Mwindadi Baule, amesema hayo wakati wa chakula cha mchana walichokiandaa kwa wafanyabiashara wakubwa wa mjini Singida.

Lengo la  chakula hicho pamoja na kuimarisha mahusiano baina ya  Kampuni na wateja wake, ni kuwaelimisha wafanyabiashara  hao kulipa madenbi yao kwa wakati ili kuiwezesha Kampuni  kujiendesha na kuboresha huduma.

Amesema  kutolipwa kwa wakati kwa deni  hilo  ni moja  ya sababu zinazoleta changamoto kubwa katika kuboresha  huduma kwa wateja pamoja na kusambaza zaidi  huduma hiyo hadi  Vijijini.

Hata  hivyo amesema mikakati mbalimbali  imewekwa na kampuni hiyo ikiwemo kutumia vyombo  vya kisheria kwa ajili ya kuhakikisha kuwa kila mteja anayedaiwa analipa deni lake  mara moja.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa