SHIRIKA lisilo la
Kiserikali la PSI-Tanzania kanda ya kati,limetoa msaada wa vitanda saba maalum
kwa ajili ya kujifungulia akina mama wajawazito kwa zahanati na vituo vya afya
saba mkoani Singida.
Msaada
huo wa vitanda  vyenye jumla ya  thamani ya  zaidi ya
shilingi  milioni  sita , umezinufaisha Zahanati na vituo vya
afya  vya Isanzu, Kinampanda, Zahanati na Hospitali ya  Iambi 
wilayani  Mkalama pamoja na Sepuka, Tumaini na polisi katika  halmashauri
ya  wilaya ya Singida.
Akizungumza
katika hafla ya kukabidhi msaada huo, Mratibu wa afya ya uzazi wa PSI bibi Zena
Mgoi,amesema  msaada huo umetolewa na shirika lao baada ya kubaini 
mahitaji katika vituo hivyo vya tiba. 
Bi
Zena  amesema lengo ni kupunguza  tatizo la vitendea kazi
katika  hospitali, vituo vya  afya na Zahanatiili kuhakikisha
kuwa  wajawazito wanapata huduma bila matatizo yoyote  wakati wa
kujifungua.
Viongozi
 mbalimbali wa  vituo vya  tiba  lvilivyonufaika na msaada
huo wametoa shukurani kwa shirika hilo na kuataka wadau wengine kuiga
mfano  huo kwa kuchangia uboreshaji  sehemu za tiba.
0 comments:
Post a Comment