Home » » PSI YATOA MSAADA WA VIFAA VYA KUJIFUNGULIA

PSI YATOA MSAADA WA VIFAA VYA KUJIFUNGULIA


SHIRIKA lisilo la Kiserikali la PSI-Tanzania kanda ya kati,limetoa msaada wa vitanda saba maalum kwa ajili ya kujifungulia akina mama wajawazito kwa zahanati na vituo vya afya saba mkoani Singida.

Msaada huo wa vitanda  vyenye jumla ya  thamani ya  zaidi ya shilingi  milioni  sita , umezinufaisha Zahanati na vituo vya afya  vya Isanzu, Kinampanda, Zahanati na Hospitali ya  Iambi  wilayani  Mkalama pamoja na Sepuka, Tumaini na polisi katika  halmashauri ya  wilaya ya Singida.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi msaada huo, Mratibu wa afya ya uzazi wa PSI bibi Zena Mgoi,amesema  msaada huo umetolewa na shirika lao baada ya kubaini  mahitaji katika vituo hivyo vya tiba. 

Bi Zena  amesema lengo ni kupunguza  tatizo la vitendea kazi katika  hospitali, vituo vya  afya na Zahanatiili kuhakikisha kuwa  wajawazito wanapata huduma bila matatizo yoyote  wakati wa kujifungua.

Viongozi  mbalimbali wa  vituo vya  tiba  lvilivyonufaika na msaada huo wametoa shukurani kwa shirika hilo na kuataka wadau wengine kuiga mfano  huo kwa kuchangia uboreshaji  sehemu za tiba.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa