Home » » SERIKALI YASHAURIWA KUTUMIA PESA ZA NHIF KUJENGA MAABARA

SERIKALI YASHAURIWA KUTUMIA PESA ZA NHIF KUJENGA MAABARA

SERIKALI imetakiwa kuangalia uwezekano wa kutenga zaidi ya asilimia 40 ya fedha zinazokusanywa  katika uchangiaji  huduma za matibabu, kwa ajili ya kutumika kwenye kitengo cha maabara.
Hatua hiyo itasaidia  katika kuboresha kitengo  hicho ambacho kinatajwa kuwa huchangia zaidi ya asilimia 70 ya maamuzi  ya Daktari katika kutibu iwapo kitatoa matokeo  na takwimu sahihi   za uchunguzi wa magonjwa.
Wito  huo  umetolewa  leo na  Rais wa Chama cha  wanasanyansi wa maabara za  uchunguzi wa afya   ya  binadamu nchini bw  Sabasi Mrina, wakati akizungumza kwenye ufunguzi wa  wiki  ya maadhimisho ya wana-taaluma wa maabara ambayo mwaka huu  kitaifa inafanyika mjini Singida.
Bw Mrina  amesema ingawa inaaminika kuwa kitengo cha maabara ndicho  kinachokusanya fedha nyingi zaidi za uchangiaji huduma za matibabu,  lakini  chenyewe kimebaki kuwa omba-omba kutokana  kutopewa  fedha  kwa ajili ya kukiboresha ili kiweze kutoa huduma nzuri zaidi kwa wagonjwa.
Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo Kaimu Mkuu wa mkoa wa Singida Bibi Queen Mlozi amesema kuna haja  ya kuboreshwa kwa huduma  za uchunguzi wa magonjwa kutokana na umuhimu wake katika  tiba.
Wiki ya wataalamu wa maabara za afya ilianza kuadhimishwa rasmi nchini mwaka 2011, ikiwa na lengo la kutoa elimu kwa jamii  juu ya umuhimu wa kuchunguza afya,  kufanya tathimini ya utendaji kazi, changamoto zinazojitokeza na kuweka mikakati mbalimbali kwa ajili ya kuboresha kitengo hicho.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa