SERIKALI imetakiwa
kuangalia uwezekano wa kutenga zaidi ya asilimia 40 ya fedha zinazokusanywa 
katika uchangiaji  huduma za matibabu, kwa ajili ya kutumika kwenye
kitengo cha maabara.
Hatua hiyo
itasaidia  katika kuboresha kitengo  hicho ambacho kinatajwa kuwa
huchangia zaidi ya asilimia 70 ya maamuzi  ya Daktari katika kutibu iwapo
kitatoa matokeo  na takwimu sahihi   za uchunguzi wa magonjwa.
Wito  huo 
umetolewa  leo na  Rais wa Chama cha  wanasanyansi wa maabara
za  uchunguzi wa afya   ya  binadamu nchini bw  Sabasi
Mrina, wakati akizungumza kwenye ufunguzi wa  wiki  ya maadhimisho ya
wana-taaluma wa maabara ambayo mwaka huu  kitaifa inafanyika mjini Singida.
Bw Mrina  amesema
ingawa inaaminika kuwa kitengo cha maabara ndicho  kinachokusanya fedha
nyingi zaidi za uchangiaji huduma za matibabu,  lakini  chenyewe
kimebaki kuwa omba-omba kutokana  kutopewa  fedha  kwa ajili ya
kukiboresha ili kiweze kutoa huduma nzuri zaidi kwa wagonjwa.
Mgeni rasmi katika
maadhimisho hayo Kaimu Mkuu wa mkoa wa Singida Bibi Queen Mlozi amesema kuna
haja  ya kuboreshwa kwa huduma  za uchunguzi wa magonjwa kutokana na
umuhimu wake katika  tiba.
Wiki ya wataalamu wa maabara za afya
ilianza kuadhimishwa rasmi nchini mwaka 2011, ikiwa na lengo la kutoa elimu kwa
jamii  juu ya umuhimu wa kuchunguza afya,  kufanya tathimini ya
utendaji kazi, changamoto zinazojitokeza na kuweka mikakati mbalimbali kwa
ajili ya kuboresha kitengo hicho.
0 comments:
Post a Comment