Wananchi
 wa kijiji cha Puma katika wilaya ya ikungi mkoani Singida wame mkataa 
mwenyekiti  wa kijiji hicho katika mkutano wake wa kwanza na kusababisha
 diwani wa kata hiyo  kwa kushirikiana na jeshi la polisi kuingilia kati
 na kufunga mkutano kabla ya wakati ili kumnusuru asipigwe na wananchi.
Wananchi hao waliokuwa na hasira wamesema hakuna sababu ya kuwa na 
mwenyekiti ambaye wananchi hawamkubali kwa sababu katika uchaguzi 
uliopita kulikuwa na udanganyifu katika upigaji kura,kutokana na hali 
hiyo wamesema ni bora kuachana na vyama vya siasa wachague mwenye kiti 
wa kimila ili kukisaidia kijiji cha puma kupata maendeleo.
Baada ya vurugu  kuongezeka diwani wa kata hiyo kwa tiketi ya 
CCM,Bwana ramadhani kulungu ilibidi kufunga kikao hicho ili kuweza 
kumnusuru mwenyekiti wa kijiji cha puma na kuwatuliza wananchi 
ilikusitokee uvunjifu wa amani.
Mwenyekiti wa kijiji cha puma  kwa tiketi ya CCM ,Bwana Sifa Joramu
 awali ambaye alishindwa kabisa kuendesha kikao chake ,baada ya jeshi la
 polisi kuingilia kati na kuamua kumsindikiza kwa ulinzi mkali huku 
wananchi waki mzomea na kusema hawamtaki,amesema hizo ni fujo za vyama 
vya upinzani lakini yeye  atahakikisha kazi anafanya kwa sababu yeye 
ndiye aliyeshinda na kuapishwa kwa kazi ya uwenyekiti wa kijiji cha 
puma. 
Kundi la watu waliamua kumfuata na kumbeba  juu kisha kumzungusha 
mitaani Bwana Hassan Chaimbo aliye gombea kwa tiketi ya CHADEMA na 
kushindwa kwa kupata kura mianne arobaini na nne dhidi ya  Bwana Sifa 
 Joramu alishinda uwenyekiti wa kijiji cha puma kwa tiketi ya CCM katika
 uchaguzi uliofanyika mwishoni  mwaka jana na kupata kura mianne hamsini
 na saba.
 Chanzo:ITV Tanzania
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
KUELEKEA UCHAGUZI 2015: JE UNAPENDA NANI AWE KIONGOZI WAKO? JAZA FOMU HII FUPI HAPA 
0 comments:
Post a Comment