| mbunge wa Singida Kaskazin Bw Lazaro Nyalandu (kulia) akimpokea waziri wa Kilimo ,Mifugo na uvuvi Bw Mwigulu Nchemba alipofanya ziara ya kikazi wilaya ya Manyoni jana | 
| Waziri Nchemba akisalimiana na mbunge Nyalandu (kulia) | 
| Waziri wa kilimo ,mifugo na uvuvi Bw Mwigulu Nchemba akiwa ameongozana na viongozi mbali mbali kuingia ukumbi wa mkutano kati yake na wakulima wa Tumbaku Manyoni | 
| Mbunge Lazaro Nyalandu kulia akiwa na waziri wa Kilimo ,mifugo na uvuvi Bw Mwigulu Nchemba wakati akisaini kitabu cha wageni ofisi ya mkuu wa wilaya ya Manyoni mkoani Singida | 
| Waziri Nchemba akiingia ukumbi wa mkutano kati yake na wakulima wa Tumbaku manyoni | 
| Wakulima wa Tumbaku wakisalimiana na waziri Nchemba | 
| Baadhi ya madiwani wakulima wa Tumbaku manyoni wakimpokea waziri Mwigulu Nchemba | 
| Baadhi ya wakulima wa Tumbaku wakiwa ukumbi wa mkutano kati yao na waziri Nchemba | 
| Mbunge wa Singida Kaskazin Bw Lazaro Nyalandu akitambulisha viongozi mbali mbali kabla ya mkutano wa wakulima wa Tumbaku kuanza | 
| Waziri wa Kilimo , Mifugo na Uvuvi Bw Mwigulu Nchemba akizungumza na wakulima wa Tumbaku wilaya ya manyoni mkoa wa Singida jana | 
| Wakulima wa Tumbaku wakitoa kero zao kwa waziri Nchemba (hayupo pichani) | 
| Wabunge wakisikiliza kero za wakulima wa Tumbaku | 
 waziri wa Mifugo na uvuvi Bw Mwigulu Nchemba  (kushoto) akimsikiliza kwa makini Mbunge wa Singida Kaskazin Bw Lazaro Nyalandu  wakati  akieleza kilio  cha wakulima wa Tumbaku  wilaya ya Manyoni wakati wa  mkutano wa  waziri Nchemba na wakulima wa Tumbaku  uliofanyika  ukumbi wa CCM Manyoni jana
WAZIRI wa  kilimo
,mifugo na  uvuvi  Bw Mwigulu 
Nchemba amefuta michango  hewa
iliyokuwa ikichangiwa na wakulima wa Tumbaku  kwa 
UNION kwa  kupitia  kitengo 
cha AMIS huku akiagiza serikali 
ya  wilaya ya Manyoni  kuwachukulia hatua  kali aofisa 
ushirika mkoa  Andru Msafiri na
afisa  ushirika Wilaya   hiyo Bw Alfred Sekiete iwapo
watabainika  kuhusika  deni la bilioni  7 
ambalo wanadaiwa benki wakulima  wa
tumbaku.
Waziri Nchemba 
alilazimika kutoa maagizo 
hayo  baada  ya 
wakulima  wa zao hilo la
Tumbaku  kulalamikia utaratibu mbaya wa
baadhi ya  viongozi wa UNION na APEX
pamoja na baadhi ya maofisa 
ushirika   kujinufaisha  kupitia mgongo  wa 
wakulima hao.
Akitoa agizo 
hilo  jana mjini Manyoni  wakati wa 
mkutano  wa  pamoja kati yake na  wakulima wa 
Tumbaku na viongozi  mbali
mbali  wa Serikali  ya 
wilaya ya Manyoni na wabunge 
wanaotoka  wilaya ya Maeneo  yanayolimwa Tumbaku  mkoani
Singida.
Waziri Nchemba 
alisema  kuwa  baadhi 
ya mambo  ambayo serikali  ya Rais Dr John Magufuli  haipendi 
kuona ni  pamoja na  wakulima kubebeshwa mizigo mikubwa ambayo
kimsingi haiwasaidii kupiga hatua kimaendeleo 
zaidi ya  kuwatesa .
Alisema 
inashangaza  kuona   wakulima 
hao  kuendelea  kuumizwa na 
viongozi  wachache ambao  wamegeuza 
wakulima ni  kichaka cha  wao 
kujificha  kujinufaisha  kupitia wakulima.
“ Mambo  ya ajabu  sana 
hiki kitu  kinaitwa AMIS ni
kuwatoza  wakulima michango ya ajabu
ajabu  eti  wakulima 
kutozwa  dola 1200 kwa  ajili 
ya kusafirisha Tumbaku toka  Dar
es Salaam kwenda UNION   pia  wanachangia dola 10 kwa  kutunza 
kumbukumbu zao  ,dola 3 kupakia na  kushusha mara mchango kwa ajili ya ADMIN   mambo ya ajabu kabisa wakulima
wanahusika  vipi na malipo maadmin yani
wanatumia lugha  za  kijanja kijanja  kuwaibia 
wakulima ADMIN wa makundi kama yale ya Whatsap kwa wakulima  tena…sasa kuanzia leo natangaza  kufuta michango  hii isiyo na maelezo ya kutosha na
kuagiza  kujipanga upya kwa  kuwashirikisha   wakulima na taarifa  hiyo ndani ya siku 7 niipate “
Waziri chemba 
alisema  kuwa kabla ya  kuanza 
kuwatoza  wakulima hao michango
ni  vizuri  makubaliano ya  michango 
hiyo yafanyike  upya kwa
kuwashirikisha  wakulima na sio
kuendelea  kutumia taratibu  za 
zamani ambazo ni mzigo kwa 
mkulima.
Kuhusu maafisa 
ushiriki  kudaiwa  kukopa 
benki  kupitia mgongo wa  wakulima 
wa  tumbaku na  kupelekea 
wakulima hao  kudaiwa  deni  benki
 la Tsh bilioni 7 aliagiza mkuu wa  wilaya ya Manyoni kuagiza wakaguzi  na wataalam wake  kufanya 
uchunguzi  na iwapo itabainika  kuwa maofisa 
hao  walihusika na deni  hilo 
hatua  stahiki  kuchukuliwa dhidi  
Alisema  ni  kosa 
kwa maofisa  ushirika   kukopa 
kwa  udhamini  wa 
wakulima   wakati  wao si 
wazalishaji wa mazao hayo ya 
kilimo na kuwa maeneo  mengi
wakulima  walikuwa wakiwalipia madeni
benki maofisa   hao ambao huomba  mikopo kupitia vyama  vya msingi vya  wakulima na wakati mwingine hushirikiana na
benki kutoa mkopo mkubwa ili  nao waweze
kugawana .
Pia aliagiza 
UNION  kufanya kazi ya  kuwasaidia  
wakulima na sio 
kuwakandamiza   wakulima na  kuwa maeneo 
mengi nchini ambayo  UNION wapo
kumekuwa na migogoro na kero nyingi kwa 
wakulima na kuwa mazao ambayo wakulima hawana UNION kama Mahindi ,
mpunga na alizeti wakulima wanafanya 
shughuli  zao pasipo migogoro  hivyo kuzitaka UNION zinazojihusisha na  wakulima wa Tumbaku , Korosho ,pamba na mazao
mengine  kujitathimini  vinginevyo hazina maana kuwepo.
Aidha  waziri Nchemba  aliagiza benki ya CRDB kuwalipa pesa  zao 
zote wakulima  wa Tumbaku ambao
wamemaliza madeni yao ya  pembejeo  na kuendelea 
kuwadai wanaodaiwa na si vinginevyo .
Mbunge  wa Singida Kaskazini  Lazaro
Nyalandu  alisema  kuwa 
kilio  kikubwa  cha  
wakulima wa Tumbaku Manyoni ni uwepo 
wa mtu kati katika kilimo  hicho
hivyo  kuwatesa  wakulima hao na  kuwa 
UNION  na APEX  bado si ukombozi kwa  wakulima wa 
zao la Tumbaku kwani  alisema  wakulima wamekuwa wakilipwa asilimia 50 ya
mauzo ya mazao yao na benki ya CRDB  na
asilimia 50 nyingine  kushikiliwa na
benki kwa mkopo wa vyama  vyao  vya msingi hata kama mkulima  husika hadaiwi.
0 comments:
Post a Comment