Mkuu wa Wilaya ya 
Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akiwa amembeba mmoja ya mwanafunzi wa shule ya Msingi Ikungi mchanganyikoMkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akikabidhi mahitaji kwa wanafunzi walemavu mara baada ya kuwasili shule ya msingi Ikungi mchanganyiko
Baadhiya washiriki wa Kongamano wakisikiliza kwa makini mada zikiwasilishwa kwenye mdahalo
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akiwa na baadhi ya viongozi wa ngazi ya Wilaya wakati kongamano likiendelea
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akimsalimu Bi Fumbo Shishiwa aliyejifungua salama mtoto wa kiume na kumuita Magufuli
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisalimiana na wanafunzi wenye ulemavu katika shule ya msingi Ikungi mchanganyiko
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akishiriki kuandaa bustani kwa ajili ya mbogamboga zitakazotumiwa na wanafunzi wa shule ya msingi Ikungi mchanganyiko
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Ikungi akichangia mada iiliyokuwa inajadiliwa kwenye Kongamano la Kumuenzi Mwalimu J.K Nyerere kwenye Ukumbi wa Shule ya Sekondari Ikungi
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisalimia na Bi Faidha Athumani mara baada ya kumkuta akisubiri matibabu katika Kituo cha afya Ikungi
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akishiriki kuandaa bustani kwa ajili ya mbogamboga zitakazotumiwa na wanafunzi wa shule ya msingi Ikungi mchanganyiko
Baadhi ya washiriki wakifatilia kwa makini Kongamano
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akikagua Chumba cha kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya Ikungi
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akikagua Mashine ya vipimo vya magonjwa mbalimbali ikiwemo ini katika kituo cha afya Ikungi
Mkuu wa Wilaya ya 
Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akimuelekeza Mganga Mkuu wa kituo cha Afya Ikungi kuhakikisha anasimamia ujenzi wa upanuzi wa chumba cha kuhifadhia maiti
 Na Mathias Canal, Singida
 Uongozi wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida umeungana na Watanzania kote
 ulimwenguni kuadhimisha kumbukizi ya miaka 17 ya kifo cha Mwasisi wa 
Taifa na Rais wa Kwanza wa Tanzania hayati Mwalimu Julius Kambarage 
Nyerere aliyefariki dunia Octoba 14, 1999  katika Hospitali ya Mtakatifu
 Thomas huko Uingereza.
 Katika Kongamano hilo lililofanyika 
katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Ikungi limejumuisha Viongozi wa kada
 tofauti wakiwemo viongozi wa serikali, Viongozi wa Dini, Viongozi wa 
Vitongoji na vijiji, Viongozi wa siasa, Wazee wa mji wa Ikungi, Maafisa 
Tarafa na Watendaji, Madiwani, Walimu na wanafunzi ambapo wote kwa 
pamoja wamepata nafasi ya kuchangia mada na kupitisha maadhimio zaidi ya
 kumi na tano yatakayotoa taswira ya namna ya kumuenzi Mwalimu Nyerere 
mwakani.
 Mgeni rasmi katika Kongamano hilo Mkuu wa Wilaya ya 
Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu amewasihi wananchi kwa umoja wao 
kumuenzi Mwalimu Nyerere katika matendo makubwa na muhimu aliyokuwa 
anayafanya hususani misingi ya Haki, Ukweli na uwajibikaji.
 
Amewataka watanzania kuishi katika matakwa ya Mwalimu Nyerere ikiwa ni 
pamoja na kutokubali kutoa na kupokea Rushwa kwani hayo ni miongoni mwa mambo 
mengi aliyoyahubiri wakati akiwa waziri Mkuu kabla ya kujiuzulu nafasi 
hiyo na hatimaye kuyahubiri na kuyaishi kipindi akiwa Rais wa kwanza wa 
Tanzania.
 Dc Mtaturu alisema kuwa Tanganyika wakati wa uhuru 
ilikuwa na changamoto mbalimbali ikiwemo maradhi yatokanayo na magonjwa 
ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza, Pia kulikuwa na ujinga uliosababishwa na ukosefu wa elimu bora kwa kiasi 
kikubwa kwani watanganyika wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu 
walikuwa ni zaidi ya asilimia 90.
 Alisema kuwa sambamba na hayo 
pia kulikuwa na umasikini mkubwa na uliokithiri kwani asilimia kubwa ya 
watanzania walikosa mahitaji ya msingi kama vile malazi, Chakula, na Mavazi 
ambapo Mwalimu Nyerere alifanikiwa kupingana na maadui hao watatu kwa 
kuongeza udahili kwa kiasi kikubwa katika shule muhimu za Sekondari 
Kilakala, Kibaha na Mzumbe.
 Mtaturu alisema kuwa pia Mwalimu 
Nyerere alitaifisha taasisi zote za watu binafsi ili kuleta usawa katika
 jamii pamoja na kuimarisha upatikanaji mzuri wa huduma za afya katika zahanati, 
vituo vya afya, na Hospitali ili kuboresha afya za watanzania 
na kuwafanya kuweza kufanya kazi vizuri na kwa ufasaha.
 Dc 
Mtaturu Amewataka washiri wote wa Kongamano hilo na watanzania kwa 
ujumla kuendelea kuwa viungo muhimu katika kudumisha Muungano wa 
Tanganyika na Zanzibar, Kudumisha Lugha ya Kiswahili, Kukuza Utu na 
uadilifu katika kazi na jamii inayotuzunguka.
 Zaidi amesisitiza 
wakulima kwa kushirikiana na maafisa kilimo kulima kilimo chenye tija 
ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ili kuhakikisha wanakuwa na 
mavuno mengi yenye faida kubwa na kuwaongeza uchumi wao kwani wastani wa
 pato la Mtanzania aishie Wilaya ya Ikungi ni shilingi elfu mbili kwa 
siku ambapo kwa mwezi ni shilingi elfu sitini.
 Hata hivyo Dc 
Mtaturu amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa 
vitendo hususani kusimamia vyema mapato ya serikali, Kupambana katika 
misingi ya utu, haki na usawa kwa kila Raia wa nchi hii, Kupinga Rushwa 
na matumizi mabaya ya fedha za Umma.
 Kwa upande wake Kaimu Katibu
 Tawala wa Wilaya ya Ikungi Ndg Dandala Mzunguor ameyataja baadhi ya 
maadhimio yaliyojadiliwa katika kongamano hilo kuwa ni pamoja na Kupata 
viongozi wa Haki na halali katika chaguzi zetu, Jamii kuwa na moyo wa 
uzalendo na kujitolea katika kufanya kazi.
 Mengine ni kuepuka 
kejeli na dharau katika maisha ya kila siku, Kuboresha mazingira ya 
kufundishia, Jamii na viongozi kuweka miiko ya uongozi, Kudumisha umoja 
na mshikamano wa Taifa letu.
 Naye katibu wa Chama Cha Mapinduzi 
CCM Wilaya ya Ikungi Aluu Segamba amempongeza Mkuu huyo wa Wilaya kwa kuamua kumuenzi
 Mwalimu Nyerere kwa kufanya kongamano kwani imekuwa taswira njema kwa 
wakazi wa Wilaya hiyo ambao hawajawahi kushiriki katika kongamano kama 
hilo tangu kuanzishwa kwa Wilaya hiyo.
 Baadhi ya wachangiaji 
katika kongamano hilo la kumuenzi Mwalimu Julius Kambarage Nyerere 
wamependekeza kuwa na siku moja ambayo Mkuu wa Wilaya atakutana na 
wananchi wote kwa ajili ya kujadili kwa pamoja namna ya kuiboresha 
Wilaya hiyo ikiwa ni pamoja na shughuli za kijamii hususani kuboresha 
kilimo, Uchumi na Miundombinu.
 Wengine wamependekeza bendera 
kupeperushwa nusu mlingoti ni kuenzi na kutoa heshima kubwa kwa Baba wa 
Taifa kwani kufanya hivyo itakuwa njia sahihi ya kuongeza uwajibikaji na
 nidhamu ya Taifa.
 Kabla ya Kongamano hilo mkuu huyo wa Wilaya ya
 Ikungi akishirikiana na viongozi wote wa Wilaya pamoja na kamati ya 
ulinzi na usalama alitembelea Shule ya Msingi mchanganyiko Ikungi ili 
kutoa baadhi ya mahitaji kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu wakiwemo Wenye ulemavu wa ngozi, Walemavu mchanganyiko na wasioona.
 Sambamba na hayo pia amewatembelea wagonjwa katika Kituo cha afya Ikungi kwa kuzuru katika wodi za wanawake waliojifungua, sambamba na 
Wodi ya wanaume na Wanawake.
 Dc Mtaturu amemuagiza mganga Mkuu wa
 Zahanati hiyo kuhakikisha anafanya utaratibu wa kujenga Sehemu ya 
kuhifadhia maiti kutoka na sehemu iliyopo kuzidiwa kwani ina sehemu 
mbili tu za kuhifadhia maiti.
Aidha Dc Mtaturu alipotembelea kituo cha Afya cha Ikungi alipitia maagizo yake aliyowahi kuyatoa hivi karibuni ya kupanua chumba cha maabara na kuagiza kutengenezwa kwa mashine ya kupimia magonjwa mbalimbali ndani ya muda mfupi ili kuboresha huduma ya afya kwa wananchi wanaotumia kituo hicho kwa ajili matibabu.
Aidha Dc Mtaturu alipotembelea kituo cha Afya cha Ikungi alipitia maagizo yake aliyowahi kuyatoa hivi karibuni ya kupanua chumba cha maabara na kuagiza kutengenezwa kwa mashine ya kupimia magonjwa mbalimbali ndani ya muda mfupi ili kuboresha huduma ya afya kwa wananchi wanaotumia kituo hicho kwa ajili matibabu.
 Akifunga Kongamano hilo Mkuu wa 
Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu amesisitiza kuwa katika 
kumuenzi Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ni lazima kuhakikisha huduma 
za Afya, Elimu, Uchumi, Kilimo na Miundombinu zinaboreshwa.















0 comments:
Post a Comment