Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana na mkuu wa mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi alipowasili wilayani Manyoni mkoani Singida leo Februari 13, 2017.
 
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli na mke wa Waziri Mkuu Mama Mary 
Majaliwa wakilakiwa kwa furaha walipowasili katika Makazi ya Wazee 
Wasiojiweza Sukamahela wilaya ya Manyoni mkoani Singida leo Februari 13,
 2017.
 Afisa
 Ustawi wa Jamii Yeremia Ngoo akiwapa maelezo Mke wa Rais Mama Janeth 
Magufuli na mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa nyumbani kwa Bibi 
Agnes Kamota (75) walipotembelea Makazi ya Wazee Wasiojiweza Sukamahela 
wilaya ya Manyoni mkoani Singida leo Februari 13, 2017.
 Mke
 wa Rais Mama Janeth Magufuli na mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa 
wakiwa na Bibi Agnes Kamota (75) walipomtembelea nyumbani kwake katika 
Makazi ya Wazee Wasiojiweza Sukamahela wilaya ya Manyoni mkoani Singida 
leo Februari 13, 2017.
 
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli na mke wa Waziri Mkuu Mama Mary 
Majaliwa wakitembelea  Zahanati ya Sukamahela katika Makazi ya Wazee 
Wasiojiweza Sukamahela wilaya ya Manyoni mkoani Singida leo Februari 13,
 2017
 Mke
 wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa akisalimia wananchi wakati yeye na 
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli walipofanya ziara  katika Makazi ya 
Wazee Wasiojiweza Sukamahela wilaya ya Manyoni mkoani Singida leo 
Februari 13, 2017.
Mke
 wa Rais Mama Janeth Magufuli na mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa 
wakishiriki kucheza ngoma na vikundi vilivyojitokeza kuwalaki katika 
Makazi ya Wazee Wasiojiweza Sukamahela wilaya ya Manyoni mkoani Singida 
leo Februari 13, 2017.
 Mke
 wa Rais Mama Janeth Magufuli akihutubia wananchi wakati yeye na mke wa 
Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa walipotembelea Makazi ya Wazee 
Wasiojiweza Sukamahela wilaya ya Manyoni mkoani Singida leo Februari 13,
 2017.
 Waziri
 Mkuu Mama Mary Majaliwa akihutubia wananchi wakati walipotembelea 
Makazi ya Wazee Wasiojiweza Sukamahela wilaya ya Manyoni mkoani Singida 
leo Februari 13, 2017.
 Mke
 wa Rais Mama Janeth Magufuli na  mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa 
wakioneshana kielele cha kilima cha Sukamahela ambapo inasemekana ndipo 
ilipo alama ya kuonesha katikati ya nchi ya Tanzania wakati wa ziara yao
 katika Makazi ya Wazee Wasiojiweza Sukamahela wilaya ya Manyoni mkoani 
Singida leo Februari 13, 2017
 Mke
 wa Rais Mama Janeth Magufuli na mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa 
wakitoa msaada wa vyakula tani 7.5  katika Makazi ya Wazee Wasiojiweza 
Sukamahela wilaya ya Manyoni mkoani Singida leo Februari 13, 2017
 Mke
 wa Rais Mama Janeth Magufuli na mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa 
wakipokea msaada wa vyakula na vinywaji kutoka kwa Meneja wa tawi la 
Benki ya NMB Singida Bw. Abius Mlengwa katika Makazi ya Wazee 
Wasiojiweza Sukamahela wilaya ya Manyoni mkoani Singida leo Februari 13,
 2017.
Mke
 wa Rais Mama Janeth Magufuli na mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa 
wakipokea msada wa vyakula na vinywaji kutoka kwa Meneja wa Tawi la CRDB
 Manyoni Bw. Richard Karatta katika Makazi ya Wazee Wasiojiweza 
Sukamahela wilaya ya Manyoni mkoani Singida leo Februari 13, 2017. PICHA
 NA IKULU
NA MWANDISHI MAALUM
MKE
 wa Rais Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli pamoja na Mke wa Waziri Mkuu 
Mama Mary Majaliwa wametoa rai kwa Wanzania kujenga tabia ya kusaidia 
watu wasiojiweza na wenye mahitaji maalumu.
Wake
 hao wa viongozi pia wamewatahadharisha watumishi wanaofanya kazi katika
 vituo vya kulelea wazee wasiojiweza wahakikishe misaada inayotolewa na 
wadau mbalimbali inawafikia walengwa bila ya kuchakachuliwa.
Wameyasema
 hayo leo (Jumatatu, Februari 13, 2017) wakati walipotembelea Makazi ya 
Wazee wasiojiweza na walemavu watokanao na ugonjwa wa ukoma ya 
Sukamahela wilayani Manyoni Mkoani Singida.
Katika
 kituo hicho wamekabidhi tani 7.5 za vyakula mbalimbali ukiwemo mchele, 
unga wa sembe na maharage, ambapo Mama Janeth amewataka viongozi wa 
kituo kuhakikisha chakula hicho hakichakachuliwi.
Akizungumza
 na wazee wa makaazi hayo, viongozi mbalimbali na wananchi wanaozunguka 
eneo hilo Mama Janeth amesema “Naomba chakula hiki kitunzwe vizuri na 
hakikisheni kinawafikia walengwa na kisichakachuliwe hii ni sadaka,”.
Kwa
 upande wake Mama Mary amewaomba wadau mbalimbali kujitokeza na 
kuwasaidia wazee wanaoishi katika makaazi ya kulelea walemavu na 
wasiojiweza nchini kwa sababu wanakabiliwa na changamoto nyingi.
“Watanzania
 wote popote mlipo tukumbuke kutembelea vituo vya kulelea wazee kikiwepo
 na hiki tulichokitembelea leo cha Sukamahela na kutoa misaada 
mbalimbali kkwa kadri tutakavyojaaliwa,” amesema.
Awali
 Mkuu wa Makazi hayo Bw. Yeremia Ngoo alisema kituo hicho kilianzishwa 
mwaka 1974 chini ya Idara ya Ustawi wa Jamii kwa lengo la kuwasaidia 
watu wenye ukoma na wazee wasiojiweza mkoani Singida.
Bw.
 Ngoo alisema kituo hicho chenye wakazi 62 kinakabiliwa na changamoto 
mbalimbali ikiwemo ya upungufu wa wapishi ambapo kwa sasa yupo mmoja 
huku mahitaji yakiwa ni wapishi wanne. Pia nyumba nyingi ni chakavu na 
zina nyufa.
Naye
 Mwenyekiti wa Wazee waishio katika makaazi hayo, Mzee Andrea Yohana 
aliwashikuru wake hao wa viongozi na kuwaomba waendelee na moyo huo wa 
kusaidia watu wasiojiweza.


0 comments:
Post a Comment