Mkuu 
wa Mkoa wa Singida Mhe. Dkt. Rehema Nchimbi akipanda viazi lishe katika 
shamba la Mkulima wa viazi katika kijiji cha Nkungi Wilayani Mkalama 
katika ziara yake wilayani humo.
Katibu
 Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Angelina Mageni Lutambi akipanda viazi 
lishe katika shamba la Mkulima wa viazi katika kijiji cha Nkungi 
Wilayani Mkalama.
Mkuu 
wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Jakson Masaka akishiri kupanda viazi lishe 
katika shamba la Mkulima katika kijiji cha Nkungi Wilayani humo.
Mkuu
 wa Mkoa wa Singida Mhe. Dkt. Rehema Nchimbi au “mama Nchimbi” kama 
anavyojulikana jana amefanya ziara ya kikazi Wilaya ya Mkalama na 
kuagiza watendaji kusimamia miradi kwa umakini kwakuwa hataki kusikia 
mradi wowote uko chini ya kiwango.
Dkt. 
Nchimbi amesema msamiati chini ya kiwango hataki kuusikia kwakuwa umekua
 ukifanya watendaji kuwa wazembe na kuongeza kuwa hatua kali 
zitachukulkiwa kwa viongozi wote ambao hawatasimamia ipasavyo 
utekelezaji wa maelekezo hayo.
Ameongeza
 kuwa watendaji wamekuwa wakiilalamikia serikali na kuirudisha nyuma kwa
 kutotekeleza majukumu yao ipasavyo na hivyo kupelekea wananchi kuona 
serikali haifanyi chochote wakati inaleta pesa nyingi za miradi 
mbalimbali ambapo jukumu la watumishi ni kusimamia miradi ili ifanye 
kazi ipasavyo.
Dkt. 
Nchimbi amesema viongozi wote kabla ya kusaini mikataba yoyote ya 
halmashauri wanapaswa kukiri thamani ya mali zao zinazohamishika na 
zisizohamishika ili kama mradi utatekelezwa chini ya kiwango, mali zao 
zitumike kufidia pesa ya serikali iliyopotea.
“Mradi
 wakati unajengwa Mkurugenzi, Mwenyekiti wa halmashauri na wataalam 
wanauangalia bila kusema chochote, ukikamilika ndio wanakuambia 
umejengwa chini ya kiwango, kuanzia sasa sitaki kusikia msamiati wa 
‘chini ya kiwango’ na endapo ikitokea chini ya kiwango tutahakikisha 
fedha ya serikali inarudi”, amesema Dkt. Nchimbi.
Aidha 
katika kikao hicho na watumishi wote wa halmashauri hiyo amewaagiza 
wakuu wote wa shule za msingi na sekondari kuwaruhusu wanafunzi ambao 
hawana sare kuanza masomo huku utaratibu wa kuwafuatilia wazazi watimize
 majukumu yao ukiendelea.
“ 
Baada ya elimu kuanza kutolewa bure, changamoto nyingine iliyobakia kwa 
baadhi ya wazazi ni uwezo wa kuwashonea watoto wao sare za shule, sasa 
ninaagiza wakuu wa shule za sekondari na Msingi wote Wilayani hapa 
kuwaruhusu watoto hao waingine madarasani hata kama hawajavaa sare za 
shule ili wasikose haki yao ya msingi kwa sababu ya sare tu”, ameagiza 
Dkt. Nchimbi.
Awali 
kabla ya kuzungumza na watumishi Dkt. Nchimbi alifanya ziara katika 
mashamba ya wakulima ili kujionea na kushiriki na wananchi shughuli za 
kilimo hasa mashamba ya viazi katika kijiji cha Nkungi na mashamba ya 
mtama katika kijiji cha Ilunda wilayani humo.
Dkt. 
Nchimbi akiwa katika shamba la mkulima wa viazi lishe katika kijiji cha 
Nkungi alipanda viazi na kuhamasisha wananchi wengine walime mazao 
ambayo yanatumia maji kwa ufanisi kama vile viazi, mihogo, matama na 
uwele kutoka na mabadilike ya tabia nchini ili kujihakikishia uwepo wa 
chakula.
Amewataka
 watendaji hasa wa kada za kilimo na ufugaji kuacha kufanya kazi kwa 
mazoea hasa kuandaa taarifa za makaratasi bali wawatembelee wakulima na 
wafugaji katika maeneo wanayofanya shughuli zao ili waweze kutoa ushauri
 kwa kupata picha halisi.“Sipendi kiongozi anayesema yupo karibu na 
wananchi kwa sababu hatuwezi kupima ukaribu uliopo hivyo ni vyema 
kuanzia sasa tuache kuwa karibu na badala yake tuwe pamoja nao”, amesema
 Dkt. Nchimbi.
 

0 comments:
Post a Comment