Na Nathaniel Limu Singida.
Halmashauri
 ya manispaa ya Singida inatarajia kutumia zaidi ya shilingi 13.1 
bilioni, kwa ajili ya kugharamia miradi mitatu ya uimarishaji miji 
(ULGSP) inayogharamia na benki ya dunia.
Hayo
 yamesemwa juzi na Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Singida 
Bravo Kizito Lyapembile, wakati akizungumzia kwenye hafla ya sherehe ya 
kusaini mkataba baina ya manispaa, washauri na mkandarasi 
atakayetekeleza miradi hiyo.
Amesema
 wamefikia hatua hiyo ya kusaini mkataba baada ya taratibu zote za 
kisheria za manunuzi kukamilika na kuongeza kuwa miradi hiyo ni ya 
ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilometa 5.75 kwa kiwango cha lami.
 “Barabara
 hizo ni pamoja na ile inayoanzia kituo cha mafuta Namfua hadi ofisi ya 
Mamlaka ya mapato (TRA) ambayo itapanuliwa na kuwa mbili (double road). 
Nyingine ni ile inayoanzia ofisi za TRA hadi makazi ya askofu wa kanisa 
la katoliki (barabara ya Kinyeto)”, ameongeza.
Lyampembile
 amesema taratibu za manunuzi katika mkataba huu zilianza mwezi Mei 
mwaka jana na kukamilika Januari mwaka huu ambapo ujenzi huo utagharimu 
zaidi ya shilingi 12.4 bilioni.
“Leo
 hii manispaa ya Singida itatiliana saini mkataba namba 
LGA/115/SMC/2016/2017 /W/NO.1 na kampuni ya China Henan International 
Co-operation Group Co.LTD (CHICO) ya jijini Dar-es-salaam. Ujenzi huo 
utakamilika baada ya miezi 12”, alifafanua zaidi.
Amesema
 CHICO atasimamiwa na  kampuni ya Luptan Consultants Ltd ya jijini 
Dar-es-salaam kwa gharama ya shilingi 648.3 milioni na itakamilika baada
 ya miezi 15. Mkataba wa mradi huo ni LGA/115/SWMC/2016/2017/C/No.02.
“Vile
 vile tutatekeleza mradi mwingine wa uandaaji wa mpango mkakati wa miaka
 mitano wa mansipaa yetu ya Singida.Mradi huu wenye mkataba 
LGA/115/SMC/2016/2017/C/No.03 una   thamani ya zaidi ya shilingi 55.9 
milioni.Mradi huu utatekelezwa na mshauri mwelekezi chuo cha mipango 
Dodoma, Titus Mwageni”,alisema.
Sherehe
 hiyo ya utiaji saini mikataba hiyo,zilihudhuriwa na mkuu wa wilaya ya 
Singida Elias Tarimo na mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Rehema Nchimbi.
Dk.Nchimbi
 Alitumia fursa hiyo kuyaomba mashirika ya TANESCO,TTCL na mamlaka ya 
maji (SUWASA) kutoa ushirikiano na mkandarasi,ili miundo mbinu yao 
isikwamishe utekelezaji wa mradi huo mkubwa ambao 
utakapokamilika,utabadilisha madhari ya mji wa Singida.
0 comments:
Post a Comment