Home » » Kamati yaagiza waachimbaji, mwekezaji kutafuta suluhu

Kamati yaagiza waachimbaji, mwekezaji kutafuta suluhu


Gasper Andrew,
Singida 
KAMATI ya Ulinzi  na Usalama  ya Wilaya ya Iramba, mkoani Singida, imewataka wachimbaji wadogo wa dhahabu katika eneo la Sekenke wilaya humo,  kufikia mwafaka baina yao na mwekezaji mwenye leseni, vinginevyo sheria ichukue mkondo wake.

Kaimu Mwenyekiti wa  kamati hiyo,  Edward Ole Lenga, alisema agizo hilo linafuatia kushindikana kwa jitihada za kuzisuluhisisha pande hizo kwa njia ya mazungumzo.

 Ole Lenga alisema kushindikana kwa jitihada hizo kumetokana na kitendo cha wachimbaji wadogo, kugoma kusaini makubaliano  kati yao na mwekezaji  John Bina, ambaye amekubali kuingia ubia na  wachimbaji hao katika eneo la leseni yake.

 Ole Lenga ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Singida alisema hatua hiyo imeilazimisha kamati hiyo kuwataka wachimbaji hao, kufikia makubaliano nje ya mazungumzo rasmi.

Alisema vingine, Serikali itachukua hatua za kisheria  kwa mujibu wa taratibu, kanuni na sheria za madini nchini.


Kauli hiyo inakuja wakati Kamishina Msaidizi wa Madini  katika Kanda ya Kati,  Manase  Mbasha, akiwa amesema  wachimbaji hao wakiendesha  shughuli zao kinyume cha sheria na kwamba wanapaswa kushtakiwa.

Wachimbaji wadogo katika eneo la Sekenke, amegoma kuondoka katika eneo  hilo wala kuingia ubia na mwenye leseni,kwa madai kuwa leseni  yake inataja eneo la Mgongo na si Sekenke.
Chanzo: Mwananchi




0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa