Home » » Singida wadhibiti kideri

Singida wadhibiti kideri


na Hillary Shoo, Singida
SERIKALI imefanikiwa kudhibiti ugonjwa hatari wa mdondo, maarufu kama ‘kideri’ mkoani hapa, unaoua kwa wingi kuku wa kienyeji, katika halmashauri ya wilaya Singida.
Hayo yalibainishwa juzi na Mkurugenzi wa Maabara Kuu ya Taifa ya jijini Dar es Salaam, Dk. Sachindra Das, wakati akitoa taarifa ya ugonjwa huo, kwenye ukumbi wa chuo cha maendeleo mjini hapa.
Dk. Das alisema kuwa hali hiyo imeifanya halmashauri hiyo na Tanzania kwa ujumla kuongoza katika kudhibiti ugonjwa huo kati ya nchi nne za Afrika, zilizoshiriki kampeni hiyo ya chanjo.
Mkurugenzi huyo, alizitaja nchi zingine zilizoshiriki kampeni hiyo iliyodumu kwa miaka mitatu na kutarajiwa kumalizika Desemba mwaka huu, kuwa ni Zambia, Malawi na Msumbiji.
Alisema kampeni hiyo ilisimamiwa na kamati ya uratibu, mradi wa kitaifa udhibiti wa ugonjwa wa mdondo, kupitia Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, kwa kushirikiana na nchi ya Australia.
Aidha, mmoja wa wafugaji wa kuku wa kienyeji katika wilaya hiyo, Madai Njau, alisema kuwa kabla ya chanjo hiyo kuanza kutolewa, alikuwa akipoteza kuku wengi kutokana na kufa kwa ugonjwa huo.
Njau alifafanua kuwa baada ya kuzingatia sharti la chanjo, hivi sasa ananufaika kwa kiwango kikubwa na kuku wa kienyeji, ambao huuza mayai na kuku kwa wafanyabiashara wa jumla
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa