Home » » Magunia ya mkaa 311 yaliyovunwa kinyemela yakamatwa Singida

Magunia ya mkaa 311 yaliyovunwa kinyemela yakamatwa Singida

WAKALA wa huduma za Misitu  nchini  katika  halmashauri ya wilaya ya Singida,amefanikiwa kukamata magunia ya mkaa 311 yenye thamani ya zaidi ya shilingi 5.2 milioni, ambayo yamevunwa kinyume na sheria.

Meneja wa wakala huyo wilayani Singida bwana Hashimu Kativo, amesema magunia hayo wameyakamata  mapemawiki hii katika msako mkali unaoendelea wa kuwakamata wafanyabiashara na watu wengine wanaouza  mazao ya misitu na nyuki kinyume na sheria za  nchi.

Amesema  magunia hayo yamekamatwa katika kijiji cha Tupendane kata ya Mang’onyi baaada ya kukuta magunia hayo yakiwa yamekusanywa  bila kuwa na kibal cha kuvuna wala leseni ya kununua na kuuza mkaa.

Hata  hivyo amefafanua kuwa wamiliki wa mkaa huo waliweza kutoroka kwenda kusikojulikana.

Bw Katiyo amesema katika ukamataji huo, pia wameharibu matanuru sita makubwa ambayo yalikuwa yakitumika kuchoma mkaa kwa ajili ya kuuza.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa