Home » » Wajumbe baraza la katiba wataka nafasi ya mgombea binafsi iondolewe kwenye katiba mpya

Wajumbe baraza la katiba wataka nafasi ya mgombea binafsi iondolewe kwenye katiba mpya

WAJUMBE wa baraza la maoni ya Katiba mpya katika Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, wamependekeza kuondolewa kwa kipengele cha mgombea huru katika nafasi za udiwani, ubunge na Raisi.
Wajumbe  hao wamesema kuwa ni vyema wagombea wote wa nafasi hizo wakatokana na vyama vya siasa, ili kupunguza uwezekano wa kumuingiza madarakani kiongozi ayesiyekuwa na maadili mazuri.
Wakizungumza kwenye kikao cha  baraza  la maoni ya katiba mpya wilaya ya Ikungi mkoani Singida leo,  baadhi ya wajumbe wamesema  wagombea wanaotokana na vyama vya siasa hupigiwa kura za  maoni na kuchunjwa kwenye vikao kabla ya  kuwepewa tiketi ya kuwania nafasi husika.
Wamesema kitendo cha kuruhusu mgombea huru,  kinaweza kusababisha watu wenye ushawishi mkubwa wa kifedha kutumia vibaya fursa hiyo kununua uongozi  na kuingiza nchi kwenye  utawala wa kiditeta.
Hata hivyo Mwenyekiti wa kikao hicho Ali Salehe amesema kuwa  kuondolewa kwa kipengele hicho,  pia kunaweza kuwanyima fursa baadhi ya wagombea  wazuri wanaoshindwa kupambana na wenye  fedha katika ngazi za vyama.
Baraza la maoni  ya katiba mpya Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida lenye wajumbe zaidi ya 100 limemaliza vikao vyake  vya siku mbili kwa kutoa mapendekezo mbalimbali katika rasimu hiyo ya Katiba.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa