Meneja
 wa shirika la SEMA, Ivo Manyanku, akizungumza kwenye uzinduzi wa siku 
ya kunawa mikono duniani, siku ya choo duniani na wiki ya usafi wa 
mazingira nchini uliofanyika katika kijiji cha Tulya wilaya ya Iramba. 
Kulia mwenye miwani ni mkuu wa wilaya ya Iramba,Yahaya Nawanda.
Na Nathaniel Limu, Iramba
SHIRIKA
 lisilo la kiserikali la Sustainable Environment Management Action 
(SEMA),linatarajia kutumia zaidi ya shilingi 396 milioni kugharamia 
utekelezaji wa mradi wa usafi mashuleni na mazingira kwa ujumla,katika 
shule saba ba kata saba za wilaya ya Iramba.
Fedha hizo ni ufadhili kutoka shirika la WaterAid Tanzania.
Hayo
 yamesemwa na meneja wa SEMA,Ivo Manyanku, wakati akizungumza kwenye 
uzinduzi wa siku ya kunawa mikono duniani,siku ya choo duniani na wiki 
ya usafi wa mazingirav nchini, iliyofanyika katika kijiji cha Tulya 
wilayani Iramba.
Alitaja
 baadhi ya malengo ya mradi huo, kuwa ni pamoja  na kuhamasisha na 
kuelimisha wanafunzi na jamii kwa jumla namna bora ya kunawa mikono.
Mkuu
 wa wilaya ya Iramba mkoa wa Singida,Yahaya Nawanda, akizungumza kwenye 
hafla ya uzinduzi wa siku ya kunawa mikono duniani, siku ya choo dunia 
na wiki ya usafi wa mazingira nchini uliofanyika kimkoa katika kijiji 
cha Tulya wilayani humo.
“Pia
 kuwaelimisha wanafunzi wa kike waliopevuka (kuvunja ungo) njia bora 
zitakazowasaidia kuwa wasafi kipindi chote cha siku zao za 
hedhi”,alifafanua Ivo na kuongeza kwa kusema;
“Shughuli
 zingine ni ujenzi wa vyoo bora na kuwahamasisha wanafunzi na jamii kwa 
ujumla kuvitumia kikamilifu.Tutawaelimisha na kuwaahamasisha kunawa 
mikono pindi wanapotoka chooni kujisaidia”.
Kwa
 upnde wake afisa afya wa wilaya ya Iramba,Yohana Dondi,alisema kuwa 
wilaya ya Iramba ina kaya zenye vyoo bora ni aslimia 42,vyoo kubalika 
52,vyoo visivyokubalika asilimia 18 na bila vyoo,ni aslimia sita.
Kwa
 mujibu wa afisa huyo,nchi zinazoendelea,asilimia 70-80 ya maradhi 
yote,yanasababishwa na maambukizi yatokanayo na vinyesi,hivyo kuwa ni 
kisababishi namba moja cha vifo.
Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu,ni Choo bora na mikono safi kwa afya bora,heshima na usawa”.
Spider
 man kutoka Temeke jijini Dar-es-salaam akitoa burudani ya kutembea juu 
ya waya kwenye hafla ya uzinduzi wa siku ya kunawa mikono duniani, siku 
ya choo duniani na wiki ya usafi wa mazingira nchini iliyofanyika katika
 kijiji cha Tulya wilaya ya Iramba.
Mkuu
 wa wilaya ya Iramba mkoa wa Singida,Yahaya Nawanda (wa nne kutoka 
kushoto) akitoa maelekezo juu ya ujenzi wa choo bora cha shule ya msingi
 Tulya.Wa tatu kushoto ni meneja wa shirika la SEMA,Ivo Manyanku.
Baadhi
 ya wakazi wa kata ya Tulya,waliohudhuria uzinduzi wa siku ya kunawa 
mikono duniani,siku ya choo duniani na wiki ya usafi wa mazingira nchini
 uliofanyika katika kijiji cha Tulya wilaya ya Iramba.(Picha zote na 
Nathaniel Limu).
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
0 comments:
Post a Comment