Home » » CHADEMA YAKOMBA 350 KWA NYALANDU

CHADEMA YAKOMBA 350 KWA NYALANDU

 CHADEMA yakomba 350 kwa Nyalandu
 CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimefanya mkutano mkubwa na kujipatia wanachama wengi mahali panapodaiwa kuwa ngome ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Singida Kaskazini, jimbo linaloongozwa na Waziri wa Utalii na Maliasili Lazaro Nyalandu.
Katika mkutano huo uliofanyika juzi katika Kijiji cha Msange na kuhutubiwa na naibu katibu mkuu wa CHADEMA Zanzibar Salum Mwalimu, ambapo zaidi ya wanachama 350 walikabidhiwa kadi pamoja na kuapishwa kiapo cha uzalendo kwa ajili ya kuwajengea ujasiri.
Mwalimu aliwaambia wanachama hao kuwa kiapo hicho cha cha kuwajengea ujasiri, ni kwa ajili ya kujiunga na kundi la watanzania wanaopigania haki na matumaini ya taifa lao.
Alisema operesheni inayoendelea iliyopewa jina la Operesheni Delete CCM (ODC) imelenga kuwafikia watanzania wote na kuwapatia ujumbe wa namna sera na mikakati ya CCM ilivyoshindwa na kwamba kinastahili kuondolewa madarakani kuanzia katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Disemba 14 mwaka huu na mkuu mwakani.
“Ndugu zangu nimefurahi leo (juzi) nimefika katika jimbo linaloongozwa na Nyalandu ambaye ni mbunge wenu … nilikuwa natamani kufika hapa  ili nione mlivyo na  maendeleo kwa kuwa mbunge wenu ni mtu wa maraha nadhani anaweza kumshinda hata Rais Kikwete kwa kwenda nje kufanya utalii” alisema Mwalimu na kuongeza
“Nilijua wenzetu kwa namna mbunge wenu alivyo, ninyi mtakuwa na huduma bora za afya, elimu, barabara na maji kumbe hakuna kitu … lakini sasa nadhani meonyesha kuondoa CCM, nafikiri hali kama mbunge wenu ameiona, ni salamu tosha kwa chama chake kujiandaa na kufungasha virago katika ofisi za serikali ifikapo mwakani. 
Chanzo;Tanzania daima
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa