CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimefanya mkutano mkubwa
 na kujipatia wanachama wengi mahali panapodaiwa kuwa ngome ya Chama cha
 Mapinduzi (CCM) Singida Kaskazini, jimbo linaloongozwa na Waziri wa 
Utalii na Maliasili Lazaro Nyalandu.
Katika mkutano huo uliofanyika juzi katika Kijiji cha Msange na 
kuhutubiwa na naibu katibu mkuu wa CHADEMA Zanzibar Salum Mwalimu, 
ambapo zaidi ya wanachama 350 walikabidhiwa kadi pamoja na kuapishwa 
kiapo cha uzalendo kwa ajili ya kuwajengea ujasiri.
Mwalimu aliwaambia wanachama hao kuwa kiapo hicho cha cha kuwajengea 
ujasiri, ni kwa ajili ya kujiunga na kundi la watanzania wanaopigania 
haki na matumaini ya taifa lao.
Alisema operesheni inayoendelea iliyopewa jina la Operesheni Delete 
CCM (ODC) imelenga kuwafikia watanzania wote na kuwapatia ujumbe wa 
namna sera na mikakati ya CCM ilivyoshindwa na kwamba kinastahili 
kuondolewa madarakani kuanzia katika uchaguzi wa serikali za mitaa 
unaotarajiwa kufanyika Disemba 14 mwaka huu na mkuu mwakani.
“Ndugu zangu nimefurahi leo (juzi) nimefika katika jimbo 
linaloongozwa na Nyalandu ambaye ni mbunge wenu … nilikuwa natamani 
kufika hapa  ili nione mlivyo na  maendeleo kwa kuwa mbunge wenu ni mtu 
wa maraha nadhani anaweza kumshinda hata Rais Kikwete kwa kwenda nje 
kufanya utalii” alisema Mwalimu na kuongeza
“Nilijua wenzetu kwa namna mbunge wenu alivyo, ninyi mtakuwa na 
huduma bora za afya, elimu, barabara na maji kumbe hakuna kitu … lakini 
sasa nadhani meonyesha kuondoa CCM, nafikiri hali kama mbunge wenu 
ameiona, ni salamu tosha kwa chama chake kujiandaa na kufungasha virago 
katika ofisi za serikali ifikapo mwakani. 
Chanzo;Tanzania daima 
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
0 comments:
Post a Comment