Mwalimu mkuu wa shule ya msingi 
Kibaoni mjini Singida, Sundi Samike, akizungumza kwenye hafla ya 
kukabidhi choo bora chenye matundu nane chenye thamani ya zaidi ya 
shilingi 16 milioni zilizotolewa na MO Dewji Foundation (shilingi 14 
milioni) na Doris Mollel Foundation shilingi 2.3 milioni).
Mwakilishi wa Mo Dewji Foundation
 mkoani Singida, Duda Mughenyi, akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi 
choo bora chenye matundu nane shule ya msingi Kibaoni mjini Singida, 
chenye thamani ya zaidi ya shilingi  milioni 16. Duda amewataka wakazi 
wa manispaa ya Singida, kujenga utamaduni wa kuchangia kwa hali na mali,
 uboreshaji wa mazingira ya shule, ili kuvutia wanafunzi kupenda shule.
Mkurugenzi wa Doris Mollel 
Foundation ya jijini Dar-es-sa-laam, Doris Mollel, akizungumza kwenye 
hafla ya kukabidhi choo bora chenye matundu nane ya shule ya msingi 
Kibaoni mjini Singida chenye thamani ya zaidi ya shilingi 16 milioni, 
kati ya fedha hizo, Mo Dewji Foundation imetoa shilingi 14 milioni na 
Doris Foundation shilingi 2.3 milioni.
Mwakilishi wa Mo Dewji Foundation
 mkoani Singida, Duda Mughenyi, (wa tatu kulia) akiteta jambo na 
Mkurugenzi wa Doris Mollel Foundation, Doris Mollel (wa pili kulia) 
wakielekea kuzindua choo bora kipya cha shule ya msingi Kibaoni.
Mwakilishi wa MO Dewji mkoani 
Singida, Duda Mughenyi, (wa pili kushoto) na Mkurugenzi wa Doris Mollel 
Foundatin, Doris Mollel (wa tatu kushoto) kwa pamoja  wakizindua choo 
bora kipya cha shule ya msingi Kibaoni chenye thamani ya zaidi ya 
shilingi 16 milioni. MO Dweji Foundation imechangia shilingi 14 milioni 
na Doris Mollel, shilingi 2.3 milioni.
Jengo la choo bora chenye matundu
 nane kilichojengwa kwa thamani ya zaidi ya shilingi 16 milioni kwa 
ushirikiano wa MO Dewji Foundation na Doris Mollel Foundation 
kitakachotumiwa na wanafunzi 842 wa shule ya msingi Kibaoni mjini 
Singida. (Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
WAZAZI/WALEZI wakazi wa  halmashauri
 ya manispaa ya Singida, wamehimizwa kujenga utamaduni wa kuchangia kwa 
hali na mali uboreshaji wa mazingira ya shule, kama njia moja wapo ya 
kuwavutia wanafunzi kuhudhuria shule.
Wito huo umetolewa na Mwakilishi wa 
MO Dewji Foundation mkoa wa Singida, Duda Mughenyi, wakati akizungumza 
kwenye hafla ya kukabidhi choo bora chenye matundu  nane chenye  thamani
 ya zaidi ya shilingi milioni 16 kwa shule ya msingi Kibaoni mjini hapa,
  yenye jumla ya wanafunzi 842, kati yao wavulana ni 377 na wasichana ni
 465.
Alisema uzoefu unaonyesha kwamba 
mazingira ya shule yakiwa safi, vifaa vya kufundishia na kujifunzia 
viwepo vya kutosha , maji safi na salama yawepo na vyoo bora 
vinavyokidhi mahitaji, hatua hiyo huwajengea mazingira mazuri wanafunzi ,
 kujiendeleza kielimu.
Akifafanua, alisema shule ya msingi 
ya Kibaoni ilikaribia kufungwa kutokana na kukosa vyoo kwa ajili ya 
wanafunzi na wanafunzi,lakini Dewji Foundation na Doris Mollel 
Foundation, ilinusuru shule hiyo isifungwe baada ya MO Dewji Foundation 
kutoa shilingi 14 milioni na Doris Mollel kutoa shilingi 2,300,000.
Duda alitumia nafasi hiyo kuwataka wanafunzi wakitunze na kudumisha usafi wa choo hicho ili kiweze kutumika kwa muda mrefu.
Kwa upande wake Doris Mollel (Miss 
Singida 2014), alisema Foundation yake itaendelea kufadhili sekta ya 
elimu mkoani Singida kama njia ya kuwashukuru wakazi  mkoani hapa kwa 
kumsapoti na kufanikisha kushinda nafasi ya Miss Singida mwaka jana.
Awali Mwalimu mkuu wa shule ya 
msingi Kindai tarafa ya Mungumaji iliyoanzishwa mwaka 1975,Sundi 
Samike,alishukuru uongozi wa Mo Dweji Foundation na Doris Mollel 
Foundation, kwa kuifadhili shule hiyo ujenzi wa choo na kuinusuru 
kufungiwa.
“Nitumie nafasi hii pia kulipongeza 
shirika la WaterAid Tanzania kwa uamuzi wake wa kufadhili ujenzi wa vyoo
 bora ambao ujenzi wake tayari umeishaanza.Aidha,nitoe wito kwa 
wazazi,wasaidie kwa hali na mali kuharakisha ujenzi huu”,alisema.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

