Kaimu msimamizi wa uchaguzi jimbo la Singida mjini, Gerald Muhabuki Zephyrin,akizungumza na Modewjiblog juu ya uchaguzi ubunge jimbo la Singida mjini.(Picha na Gasper Andrew).
Na Nathaniel Limu, Singida
PINGAMIZI
 lililowekwa na Chama Cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA),jimbo la 
Singida mjini, dhidi ya mgombea wa CCM Mussa Ramadhan Sima kuwa fomu 
zake haziko sawa kwa mujibu wa kanuni,taratibu na sheria za 
uchaguzi,limetupiliwa mbali kwa madai kwamba halina mashiko.
Akizungumza na mwakilishi wa Modewjiblog
 ofisini kwake, kaimu msimamizi wa uchaguzi jimbo la Singida 
mjini,Gerald Muhabuki Zephyrin, alisema kuwa CHADEMA iliwasilisha 
pingamizi kwamba barua ya kumthibitisha Sima kugombea ubunge kupitia 
tiketi ya CCM, imesainiwa na mtu ambaye hakubaliki kisheria.
Akifafanua,
 alisema mgombea wa jimbo la Singida mjini kupitia CHADEMA, Msindai 
Mgana Izumbe, amelalamikia barua hiyo kuwa imesainiwa na  Mary Maziku, 
kwa madai sio katibu halisi wa mkoa wa Singida.
Gerald
 alisema katika  kujiridhisha kama kweli Maziku sio mtu stahiki wa 
kumuthibitisha mgombea wa CCM kwenye nafasi ya ubunge jimbo la Singida 
mjini,aliwasiliana na makao makuu CCM Lumumba jijini Dar-es-salaam,na 
kujibiwa kwa barua kwamba Maziku ndiye katibu wa CCM mkoa wa Singida.
“Mgombea
 Msindai ambaye alikuwa mwenyekiti CCM mkoa hadi kumalizika kwa mchakato
 wa kura za maoni,katibu wake wa mkoa kwa wakati huo, alikuwa Mary 
Chatanda ambaye nafasi yake imechukuliwa na Mary Maziku kipindi cha 
mchakato wa kura za maoni unaendelea.Maziku ndiye aliyesaini barua ya 
kumthibitisha Sima”,alifafanua zaidi.
Katika
 hatua nyingine,Gerald ambaye ni mkuu wa idara ya utumishi na utawala 
manispaa ya Singida,amesema kuwa aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la 
Singida mjini,Victoria John Msusu kupitia UPDP,ameeguliwa kwenye 
kinyang’anyiro hicho baada ya kushindwa kutimiza masharti ikiwemo 
kushindwa kuwasilisha fomu kwa wamadai na kushindwa kulipa ada ya fomu 
shilingi 50,000.
Msimamizi
 amewataja wagombea wa ubunge wa jimbo la Singida mjini waliopitishwa na
 chama kwenye mabano kuwa ni ni pamoja na Sima (CCM),Jeremia Paulo 
Wandili (ACT Wazalendo),Msindai Mgana Izumbe (CHADEMA) na Mwanamvua John
 Haji (CUF).
Alisema
 kampeni zimeishaanza vizuri kwa amani na utulivu mkubwa na amewaoomba 
wagombea kufanya kampeni kwa ustarabu na kuzingatia kanuni,taratibu na 
sheria za uchaguzi.
“Matarajio
 ya wananchi wa jimbo la Singida mjini,ni kwamba oktoba 25 mwaka 
huu,wapige kura kuwachagua viongozi wanaoamini watawaletea maendeleo ya 
kweli na si vinginevyo”, alisema Gerald.
0 comments:
Post a Comment